WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amekabidhiwa Uwanja wa Uhuru uliokuwa unakarabatiwa kwa takribani miaka mitatu.

Akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Elissante  Ole Gabriel amekabidhiwa uwanja huo uliogharimu zaidi ya bilioni 12 uliojengwa na  Kampuni ya Beijing Construction kutoka nchini China.

Nape amesema kuwa, uwanja huu mbali na kutumika kwa ajili ya michezo anatoa fursa kwa vyama vya michezo kuja kufungua ofisi zao kwani kuna eneo kubwa sana ambaloliko wazi.

Uwanja huo kwa sasa una uwezo wa kuchukua mashabiki 25000 watakaokuwa wameketi tofauti na awali na ukarabati huo utaudumu kwa takribani  miaka 200.
Uwanja wa Uhuru ulivyo karabatiwa na  Kampuni ya Beijing Construction kutoka nchini China.
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,Elissante  Ole Gabriel kulia akisaini baada ya kukabidhiwa uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo. aliyekaa kushoto ni mwakailishi wa   Kampuni ya Beijing Construction kutoka nchini China wakisaini mikataba kabla ya kukabidiana uwanja huo jijini Dar es Salaam leo.
 Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kukabidhiwa uwanja wa Uhuru uliokuwa ukikarabatia na kampuni kutoka nchini China.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...