Waziri wa Zamani wa Habari wa Jamhuri ya Watu wa China Zhao Qizheng akiongea na Wakuu wa
Vitengo vya Mawasiliano Serikalini kuhusu umuhimu wa Serikali kuwasiliana kimkakati na wananchi na
namna bora ya kuwasilisha taarifa kwa jamii, wakati wa kikao kazi cha kubadilishana uzoefu wa masuala
ya Mawasiliano Serikalini, leo Jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO)
Bw. Hassan Abbas.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Hassan Abbas akiongea na baadhi ya Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini mara baada ya kumalizika kwa kikao kazi baina ya Waziri wa Zamani wa Habari wa Jamhuri ya watu wa China Zhao Qizheng na Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini.
Baadhi ya Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini wakimsikiliza Waziri wa Zamani wa Habari
wa Jamhuri ya Watu wa China, Zhao Qizheng, wakati wa kikao kazi cha kubadilishana uzoefu wa masuala
ya Mawasiliano Serikalini, Leo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Zamani wa Habari wa Jamhuri ya Watu wa China Zhao Qizheng na Mkurugenzi wa Idara
ya Habari (MAELEZO) Bw. Hassan Abbas wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wakuu wa Vitengo
vya Mawasiliano Serikalini, wakati wa kikao kazi cha kubadilishana uzoefu wa masuala ya Mawasiliano
Serikalini, leo Jijini Dar es Salaam.PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...