Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
KIKOSI  cha Yanga  cha Yanga leo hii kimeendelea na mazoezi ya kujianda na mechi ya Ngao ya Hisani dhidi ya azam unaotarajiwa kuchezwa siku ya jumatano Augosti 17.

Mazoezi ya Mabingwa hao watetezi wa ligi kuu Vodacom yanafanyika katika viwanja vya Gymkhana klabu huku kikosi hicho ki knocktarajiwa kuwakosa wachezaji wake kadhaa baada ya kuwa majeruhi.

Mshambualiaji wa kimataifa Donald Ngoma amerejea kikosini baada ya kuwa mapumziko kwa kipindi kirefu na akitumikia adhabu ya kadi mbili za njano za michuano ya kombe la Shirikisho Barana Afrika Na kuukosa mchezo dhidi ya Mo Bejaia.

Kocha Mkuu, Hans Van De Pluijm ameonekana kuwa  makini sana katika kuhakikisha anaendelea kuibuka na ushindi kwa mara nyingine  tena Mpaka sasa Yanga wameweza kuifunga Azam mara tatu mfululizo na kuichukua Ngao mara 5.

Wachezaji ambao ni Majeruhi ni 
Ally Mustapha anayeuguza kifundo cha kidole, Kelvin Yondani(jicho), Juma Abdul(misuli), Obrey Chila Chirwa(goti) na Vicent Andrew Dante(nyonga).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...