Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii.
BODI ya Ligi Kuu (TPLB) ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imethibitisha kuwa mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Young Africans ya Dar es Salaam na JKT Ruvu ya Pwani, uliopangwa kufanyika Jumatano Agosti 31 mwaka huu kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam imeahirishwa mpaka itakapopangiwa tarehe nyingine.

Mabadiliko hayo hayatavuruga ratiba ya mechi zinazofuata za Ligi Kuu ya Vodacom kwa timu husika.

Taarifa hiyo imekuja baada ya uongozi wa Yanga kutuma barua ya kuomba kusogezwa mbele kutokana na idadi kubwa ya wachezaji wake kujiunga na timu zao za taifa na tayari Yanga na JKT Ruvu wameshapatiwa barua za kujulishwa.

TFF imesogeza mbele mchezo huo, na utapangwa tena lini utachezwa, ligi itaendelea Septemba tatu mwaka huu kwa michezo minne kupigwa kwenye viwanja tofauti.

Mbao FC  wataikaribisha Mbeya City katika Uwanja wa CCM Kirumba, Kagera Sugar watakuwa kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Kaitaba kuialika Mwadui FC, Majimaji FC watawakaribisha Mtibwa Sugar kwenye dimba la Majimaji Songea huku JKT Ruvu wakiumana na African Lyon katika uwanja wa Mlandizi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...