Na Zuena Msuya Arusha
Serikali imekusanya mrabaha wa zaidi ya shilingi milioni
331 katika mnada wa madini ya Tanzanite
yaliouzwa kwa zaidi ya shilingi bilioni
7.56 kutoka kampuni mbili za uchimbaji
madini hayo katika eneo la Mirerani mkoani Manyara.
Akitangaza
washindi wa zabuni za kununua madini ya Tanzanite mkoani Arusha, kwa
niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Joel Bendera, Mkurugenzi wa kitengo
uthaminishaji Almas na madini ya vito(TANSORT), Ardhard Kalugendo alisema kuwa
katika mnada huo kampuni tano zilijitokeza, mbili kati ya hizo ziliuza madini
yake kwa wanunuzi mbalimbali; Kampuni tatu hazikuweza kuuza kutokana na
kutokubalina bei na wanunuzi.
Kalugendo alifafanua kuwa mnada huo ulifanyika kwa njia
ya uwazi na kushirikisha wafanyabiashara wa ndani na nje ya Tanzania.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Joel Bendera
alisema kuwa mnada huo umeiwezesha Serikali kupata mrabaha pamoja na kuzuia
utoroswaji wa madini hayo nje ya nchi uliokuwa ukiikosesha Serikali mapato yake
kwa maendeleo ya taifa.
Katika hatua nyingine Bendera aliwatoa hofu wachimbaji wa
madini ya Tanzanite katika migodi ya Mirerani mkoani Manyara kuwa kwa Serikali
imeimarisha ulinzi kwa usalama pamoja na mali zao; Pia wafanyabiara wa
Tanzanite watoe ushirikiano kwa vyombo vya usalama pale wanapoona kuna viashiria
vya uvunjifu wa amani.
Aidha aliwasihi wanunuzi na wachimbaji wa Tanzanite
kufuata sheria na taratibu za uchimbaji na ununuzi ili kuhakikisha kuwa madini
hayo adhimu yanayopatikana nchini tanzania pekee duniani yanawanufaisha
watanzania wote.
Naye Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Madini wa Wizara
ya Nishati na Madini Profesa James Mdoe alisema kuwa pamoja na manufaa
yaliopatikana katika mnada huo, Serikali itaendelea kuboresha mnada huo kwa
kuongeza muda zaidi ili kutoa fursa kwa kila
mfanyabiasha wa Tanzanite kushiriki; Vilevile kuwepo na majadiliano zaidi kati ya wauzaji
na wanunuzi wa madini ya Tanzanite ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Profesa Mdoe aliongeza kuwa lengo la Serikali katika
mnada huo ni kuwawezesha wafanyabiashara wa Tanzanite kupata matokeo
chanya na yenye tija katika shughuli
zao, pia Taifa linufaike kutokana na matokeo hayo kwa njia mbalimbali.
Mmoja wa wafanyabiashara ya madini ya Tanzanite, ambaye
ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Tanzaniteone Faisal Shuhbhai aliipongeza Serikali
kwa kuweka utaratibu huo ambao ni wa
kwanza kufanyika nchini kwakuwa utawawezesha wafanyabiashara hao kufanya
shughuli zao kwa ufanisi tofauti na ilivyokuwa hapo awali.
Faisal alisema kuwa utaratibu wa mnada utawawezesha
wafanyabiashara wa Tanzanite waliokuwa wakikwepa kodi, kulipa mirabaha kwa
wakati baada ya kuwepo kwa mpango huo ambao haukuwepo hapo awali; Aidha
utawasaidia wafanyabiara kupata bei elekezi inayoendana na soko la dunia na
hivyo kuacha kutorosha madini ya
Tanzanite nje ya Tanzania kwa madai ya kutafuta masoko.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Joel Bendera(
aliyesimama)akihutubia wakati wa kumtangaza mshindi wa zabuni ya kununua
madini ya Tanzanite, katika mnada wa madini hayo uliofanyika mkoani Arusha. Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia madini wa Wizara ya Nishati na Madini Profesa James Mdoe(wa pili kushoto), Mkurugenzi wa kitengo cha uthaminishaji
Almasi na madini ya vito, Archard Kalugendo( kulia) na Kamishna Msaidizi wa
Madini, Salim Salim( kushoto)
Baadhi ya wauzaji na wanunuzi na madini ya Tanzanite
walioshiriki katika mnada,Mkurugenzi wa Kampuni ya TanzaniteOne Faisal
Shahbhai,(kulia) Hussein Gonga( wa pili kulia) mchimbaji, Mkurugenzi Mkuu wa
Kampuni ya VGL Group ,Sunil Agrawal( wa pili kushoto), na Mmoja wa Wakurugezi
wa Kampuni ya TanzaniaOne, Rizwan Ullah
( kushoto)
Mkurugenzi wa kitengo cha uthaminishaji Almasi na madini
ya vito,Archard Kalugendo( kulia)akitangaza washindi wa zabuni za kununua
madini ya Tanzanite,mkuu wa mkoa wa Manyara Joel Bendera( wa pili kulia) Naibu
Katibu Mkuu anayeshughulikia madini wa Wizara ya Nishati na Madini Profesa James Mdoe(wa pili kushoto).
Mhandisi Juma Lunda( kulia)akitoa bahasha katika sanduku
maalum la kuhifadhia maombi ya zabuni za kununua madini ya Tanzanite katika
mnada.
Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Madini wa Wizara ya
Nishati na Madini Profesa James Mdoe,( kushoto) akishuhudia uchambuaji wa barua
za maombi ya zabuni ya kununua madini ya Tanzanite wakati wa mnada.
Huko nyuma makusanyo haya Nani alikuwa anayafhukua? Sasa Kazi Tu.
ReplyDelete