Naibu Waziri wa Afya Arusi Said Suleiman wa kwanza (kulia) akizungumza na akinamama waliohudhuria maadhimisho ya kilele cha wiki ya unyonyeshaji duniani katika kijiji cha Mwera Wilaya ya Kati Unguja.

Na Ramadhani Ali/Maelezo Zanzibar  

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) limesisitiza umuhimu kwa Tanzania kuongeza juhudi katika kuweka mikakati ya kuboresha unyonyeshaji wa watoto mara tu baada ya kuzaliwa hadi kufikia miaka miwili.

Akitoa salamau za kilele cha wiki ya unyonyeshaji duniani iliyoadhimishwa katika kijiji cha Mwera Wilaya ya kati Unguja,  Afisa Lishe kutoka  UNICEF  Dar es Salam, Elizabeth Macha  alisema utafiti wa 2014 unaonyesha  ni mtoto mmoja kati ya wawili wenye umri hadi kufiki miezi 23 wanaonyonyeshwa mara baada ya kuzaliwa kwa Tanzania.  
       
Alisema kwa Zanzibar ni asilimia 61 tu ya watoto wenye umri kati ya miaka 0-23 wanaonyonyeshwa katika muda wa nusu saa baada ya kuzaliwa na Mkoa wa Kusini Pemba upo nyuma  zaidi ukiwa na asilimia 52.

Aliongeza kusema kuwa watoto wakicheleweshwa kunyonyeshwa kwa masaa 2 hadi 23 baada ya kuzaliwa inaongeza hatari ya kufa katika siku 28 za kwanza za maisha ya mtoto kwa asilimia 40.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...