Wafanyakazi wa bandari ya Zanzibar wakishusha madeski yaliyotolewa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya wanafunzi wa Zanzibar.
Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Tanzania Salim Hassan Turky akimkabidhi sehemu ya madeski hayo Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya kuchangia madeski Zanzibar Haroun Ali Suleiman Bandarini Zanzibar.
Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Tanzania Salim Hassan Turky akizungumza na waandishi wa habari kuhusu madawati hayo wakati wa makabidhiano bandarini Zanzibar.
Picha na Mkame Mshenga -Maelezo Zanzibar.

Na Mwashungi Tahir, Maelezo Zanzibar.
JUMLA ya madawati  5,500 ikiwa ni mgao wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutoka  Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  yamewasili  Zanzibar  kwa ajili ya matumizi ya wanafunzi wa skuli za Unguja na Pemba.

Akipokea madawati hayo  bandarini  Zanzibar, Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya madawati  Zanzibar  Haroun Ali Suleiman amesema mgao huo utapunguza tatizo kubwa la madawati linalozikabili skuli nyingi hapa nchini.

Amesema kupatikana kwa madawati hayo  kutaleta faraja kwa wanafunzi na kuongeza hamasa na ari katika kujipatia elimu.

“Msaada huu utapunguza usumbufu wa wanafunzi kukaa chini kwa muda mrefu na utaongeza ufanisi kwa walimu na wanafunzi katika kusomesha na kujifunza, “alisema Mwenyekiti huyo.

Nae  Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Riziki  Pembe Juma amewashukuru Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kusimamia kupatikana madawati hayo na ameeleza matumaini yake ya kupatikana msaada zaidi wa madeski.

 Amewaomba wasamaria wema kujitokeza kuunga mkono juhudi za Serikali katika kukabiliana na tatizo la madawati kwa kutoa michango yao kupitia Kamati ya Taifa ya Madawati ya Zanzibar.  

Aidha  amewaomba walimu wakuu wa skuli zitakazopata madeski hayo kuwapa elimu wanafunzi  jinsi ya kuyatunza  ili yaweze kudumu kwa muda mrefu.

Sambamba na hayo Spika wa Baraza la Wawakilishi  Zuberi Ali Maulid alisema kupatikana kwa madeski hayo  ni faraja  kwa baraza hilo kwani suala hilo linazungumzwa sana na tumeanza kuona mafanikio  yake.

Amesema kupatikana kwa msaada huo ni jambo la kupigiwa mfano kwa wabunge kwani wabunge  waliopita  hawajawahi kufanya jambo kama hilo. 

Makamo Mwenyekiti wa wa Bunge Salim Hassan Turky ambae ni Mbunge wa Jimbo la Mpendae kwa niaba ya wabunge wenziwe amesema  madawati hayo ni mchango   wa bunge  uliotokana na pesa za bajeti zilizobakia katika  bajeti iliyopita.

Jumla ya shilingi billion sita zimetumika kununulia madawati hayo  ambayo ni kila jimbo lilitarajiwa  kupata  madeski 300 na  kwa kuanzia kila jimbo limetapatiwa madeski 100 na mengine yatafuatia baadae.

Aidha amemshukuru Rais  wa Jamhuri ya Muungano Mh. John Pombe Magufuli kwa kutoa wazo la kutumia fedha zilizobaki za bunge  bajeti iliyopita kwa kununulia madeski hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...