Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi akifanya mazungumuzo na mmiliki wa chuo cha Mount Eagle College &University Dr. Lucas Shallua siku ya Ijumaa Septemba 3, 2016 Balozi Wilson Masilingi alipotembelea chuo hicho kilichopo Winston Salem, North Carolina.
 Mazungumuzo yakiendelea, wengine katika kufuatilia mazungumuzo hayo kutoka kushoto ni ni Afisa Uhamiaji wa Ubalozi Bwn. Abbas Missana, Dr. Dorothy Edward Shallua (mke wa Dr. Lucas Shallua), Mke wa Balozi Marystela Masilingi, na mwenyeiki wa Umoja wa Watanzania North Carolina, Bi. Gloria Alex.
 Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi akimsikiliza Dr. Lucas Shallua (kulia) alipokua amkitembeza na kumwonyesha chuo cha Mount Eagle College & University kilichopo mji wa Winston Salem, North Carolina. Wengine katika picha kutoka kushoto ni mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Watanzania North Carolina, Bi. Gloria Alex, Mke wa Balozi Bi. Marystela Masilingi, nyuma ya Balozi asiyeonekana ni Afisa Uhamiaji wa Ubalozi Bwn. Abbas Missana na Mke wa Shallua, Dr. Dorothy Edward Shallua.

Chuo cha Mount Eagle kinatoa unafuu kwa Mtanzania anayetaka kujiunga katika masomo ya Unesi na ugawaji dawa na chuo hicho kwa kukuwezesha wewe kufanyakazi hospitanini au kwenye maduka ya dawa pia wanamsomo ya mtandaoni kwa bei nafuu. Kwa maelezo zaidi usisite kuwasiliana na Dr. Lucas Shallua barua pepe Lshallua@mounteag.com 
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...