Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko akizungumza wakati wa hafla iliyowakutanisha Baraza la Madiwani na Uongozi wa Ashanti United iliyofanyika mwishoni mwa wiki na kuisaidia timu hiyo kurejea ligi na itakuwa chini ya Manispaa ya Ilala                      
 Kulia ni Diwani wa kata ya Ilala, Saadi Khimji na kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Ashanti United Almas Kasongo.
 Makamu Mwenyekiti wa Ashanti United United Almas Kasongo akizungumza na kueleza changamoto walizokuwa nazo katika kuendesha timu na kumshukuru Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko(kulia) kwa hatua nzuri waliyoifikia ya kuamua kuisaidia timu yao.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Charles Kayeko akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa timu ya Ashanti jijini Dar es Salaam.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Ilala Charles Kuyeko ameitaka klabu ya Ashanti kuhakikisha wanarejea ligi kuu kwani kwa sasa wapo nao bega kwa bega.

Hatua hiyo imekuja baada ya Manispaa ya Wilaya ya Ilala kuona umuhimu wa kuwa na timu na sasa Ashanti itakuwa chini ya Manispaa na wataisimamia kwa hali na mali.

Akizungumza na Viongozi wa Ashanti pamoja na Baraza la Madiwani,  .Charles Kuyeko amesema Ashanti ni timu kubwa kwani ina muda mrefu sana na imeweza kuhimili kujiendesha kwa fedha chache za wanachama na zimekuwa hazitoshelezi kulingana na bajeti yao ya kila mwaka.

Kuyeko amesema kuwa kuna timu nyingi sana zinazosimamiwa na Manispaa na zimekuwa zikifa ya vizuri na zaidi ukiangalia kwa timu za Ilala zinazoshiriki  ligi daraja la Kwanza ukiacha Simba na Yanga zilizowafuata kuhitaji msaada wao zaidi ya Ashanti na baraza zima la madiwani wameahidi kushirikiana nao kwa hali na mali.

Kwa niaba ya uongozi wa Ashanti United, Makamu Mwenyekiti Almas Kasongo amesema kuwa wamepokea taarifa hiyo kwa bashasha kubwa sana hasa ukifikiria walikuwa na upungufu wa bajeti ya 2016/2017 ya takribani milioni 75, na zaidi ukiachilia hilo uwepo wa Baraza la Madiwani katika timu yao ya Ashanti utaleta hamasa kubwa sana kwa watu wengine kujitokeza kuja kuisaidia.

Ashanti United imeweza kuwakutanisha baraza la Madiwani wa Manispaa ya Ilala takribani 30 na wote wameonyesha nia ya kuiunga mkono timu hiyo na kwa kuanzia kwenye hafla hiyo, Mstahiki Meya alitangaza kuanza na Milioni tano lakini watakapokutana tena watasema ni kiasi gani watakitoa na watakapokuwa na shida wasisite kupiga hodi kwake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...