Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) Bw Godfrey L. Mngereza
akizungumza katika kikao cha Mahusiano mema kati ya BASATA na Makumbusho
na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam.
Mkurugeni wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Bw Achiles
Bufure na Mratibu wa Program ya Museum Art Explosion Bw Edgar Chatanda
wakimsikiliza kwa makini Katibu Mtendaji wa BASATA Bw Godfrey L. Mngereza
(hayupo pichani)
Na SIXMUND J. BEGASHE - Makumbusho ya Taifa.
Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni imekutana na Baraza la Sanaa Tanzania
(BASATA) na kufanya mazungumzo ya namna vyombo hivi viwili vya Serikali
vitakavyo weza kudumisha mashirikiano katika shughuli za kila siku ili kuhifadhi
na kuendeleza Sanaa na Utamaduni wa Mtanzania.
Akizungumza kwenye kikao hicho Katibu Mtendaji wa BASATA Bw Godfrey L.
Mngereza ameipongeza Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni kwa kuanzisha
Program ya kila mwisho wa mwezi “Museum Art Explosion” ili kutoa nafasi kwa
wasanii wa Tanzania kuosesha kazi zao za sanaa za Ufundi na za jukwaani kitu
ambacho kinasaidia kukuza pato la msanii na pia kuutangaza Utamaduni wetu.
“Mashirikiano yetu BASATA na Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es
Salaam yatasaidia vyombo hivi hasa Makumbusho kufanya kazi za Sanaa na
Utabaduni kwa usalama mkubwa kwa kuwa BASATA itasaidia kuwamulika
wasanii wasio tambuliwa na Baraza ambao watataka kufanya maonesho kwenye
Makumbusho yetu na hasa kwenye hii program ya Museum Art Explosion”
Aliongeza Bw Mngereza.
Nae Mkurugenzi wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Bw Achiles Bufure,
ameeleza kuwa mahusiano ya BASATA na Makumbusho hiyo ni ya kihistoria
kwani BASATA ilihusika kwa kiasi kikubwa kwenye kutoa ushauri juu ujenzi wa
mradi wa Nyumba ya Utamaduni na namna itakavyo tekeleza kazi zake za
Maendeleo ya Sanaa na Utamaduni Nchini.
“Japokuwa tunatekeleza kazi zetu za msingi kama Makumbusho na Nyumba ya
Utamaduni kwa kupitia program mbali mbali za sanaa na Utamaduni lakini
tumeona ni vyema tukakutana na wenzetu wa BASATA ili watuongezee maarifa
zaidi ya namna ya kuziboresha hizi program zetu hususani hii ya MUSEUM ART
EXPLOSION maana wao ni wabobezi wa Sanaa na Utamaduni”. Alisema Bw
Bufure
Kikao hicho kilicho udhuriwa na wajumbe wa tano kutoka Makumbusho na
Nyumba ya Utamaduni na wanne kutoka BASATA kiliangazia mashirikiano
katika nyaja ya Utoaji elimu kwa Wasanii, Mawasiliano, Utafiti na Maonesho ya
kazi za Sanaa hivyo kamati ndogo ziliundwa ili zitoke na mapendekezo zaidi
yatakayo wezesha vikao vya juu kupitia na kupitisha maamudhi sahii.
Na SIXMUND J. BEGASHE Wa Makumbusho ya Taifa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...