Mkuu wa Chama cha Wafugaji Tanzania (pichani kati),Magembe Makoye akizungumza mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo jijini Dar kuhusiana na mambo mbalimbali yanayowakabili wafugaji hapa nchini,kushoto ni Mfugaji kutoka Suwambawaga,Mayunga Gamas na kulia ni Charles Mtokambati.

Bwa.Maghembe Makoye alieleza changamoto mbalimbali zinazowakabili wafugaji hao kuwa ni Ukosefu wa Maeneo rasmi ya malisho,Migogoro Baina ya Wakulima na Wafugaji,Migogoro kati ya Wafugaji na Idara ya Maliasili na Wanyamapori.Akaeleza kuwa kwa sasa kuna Mgogoro mkubwa kati ya Idara za Maliasili na Wanyamapori ndani ya Wizara ya maliasili na utalii na Wafugaji,akafafanua kuwa changamoto hizo zimekuwa sugu kutokana na kupanuka kwa maeneo ya Maliasili na kuchukua maeneo ya Wafugaji.

"Wafugaji wamekua wakifukuzwa kutoka kwenye maeneo hayo ambayo hapo awali walikuwa wakiyatumia kwa malisho,baada ya kuchukuliwa na maliasili na kuwa sehemu ya maeneo yaliyohifadhiwa.
Mkuu wa Chama cha Wafugaji Tanzania (pichani kati),Magembe Makoye akionesha baadhi ya Nyaraka kwa waandishi wa habari,zinazoeleza kukamatwa kwa ng'ombe za wafugaji hao zaidi ya elfu moja na Wizara ya Maliasili na Utalii,ambapo mahakama iliamua kuwa Maliasili na Utalii irejeshe Ng'ombe hao kwa wafugaji,ambapo mpaka sasa kwa mujibu wa taarifa ya wafugaji hao hakuna kilichofanyika mpaka sasa


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. ...makao makuu ya chama yapo Dar es Salaam. Kuna wafugaji Dar es Salaam kweli?

    ReplyDelete
  2. Bodi ya pamba - Dar
    Stamico - Dar
    Bodi ya korosho - Dar

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...