Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela leo amefungua mafunzo ya Mgambo Kata ya Wasa na kata ya Kihanga Wilayani humo, jumla ya wana mgambo 170 wameanza rasmi mafunzo, pamoja na mambo mengine watajifunza uzalendo, mbinu za kivita, utawala na usalama wa raia. DC Kasesela amesisitiza suala la usafi, kuacha ulevi, kuwa mfano wa kuigwa kwenye jamii na kuwa waaminifu. 

Akimkaribisha Mkuu wa wilaya, Mshauri wa Mgambo Mkoa wa Iringa Lt. Col. Kitta alisisitiza kuwa wanao jifunza mgambo wana fursa nyingi sana za ajira hivyo basi wajitahidi wote wamalize mafunzo. Mafunzo hayo mpaka sasa katika wilaya ya Iringa yapo Kata ya Wasa, Kihanga, Mboliboli na manispaa ya Iringa.
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akifatilia Mafunzo hayo ya Mgambo wakati alipoyafungua leo katika Kata za Wasa na Kihanga. Kulia ni Mshauri wa Mgambo Mkoa wa Iringa Lt. Col. Kitta.
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akipokea taarifa ya mafunzi hayo.
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akizungumza na Vijana wanaopatiwa Mafunzo ya Mgambo wa Kata za Wasa na Kihanga, Wilayani humo wakati alipoyafungua.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...