Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe
Luhaga Mpina amemtaka Mkuu wa Wilaya ya
Kigamboni Bw. Hashim Mgandilwa kuhakikisha fukwe zote za kigamboni zinafanyiwa
usafi na kuwa katika hali ya kuridhisha.
Naibu Waziri Mpima ameseyasema hayo leo katika maeneo ya
fukwe za kigamboni aliposhiriki katika siku ya
usafi kitaifa ya mwezi wa September.
Amesema fukwe za kigamboni ni chafu sana na usafi wa
mazingira katika mji wa kigamboni hauridhishi, “pamoja na wananchi kujitokeza
kwa wingi katika kusafisha mazingira leo fukwe ni chafu na wengine wanatuangalia
tunavyosafisha huku wakiendelea na shughuli zao, Angalia wale wavuvi kwenye mitumbwi
yao wanaendelea na kazi zao na wao ndo wachafuzi wakubwa huko baharini na nchi
kavu. “Alisema.
Mpina amemtaka mkuu wa wilaya hiyo kuwawajibisha viongozi
walioko chini yake kwa kosa la uzembe wa ufuatiliaji wa sheria ya mazingira
kabla hajawajibishwa yeye. “kiongozi mzembe afukuzwe kazi kabla haujafukuzwa
wewe na kuingia kwenye matatizo.” Alisisitiza naibu waziri Mpina.
Hata hivyo Naibu Waziri Mpina alimpongeza mkuu wa Mkoa wa Dar
es Salaam Paul Makonda kwa kuanzisha
kampeni ya upandaji miti maarufu kama ‘’MTI WANGU’’ na kuwashauri wakazi wa
jiji kushiriki Katika siku ya uzinduzi na kuahidi kuwa pamoja nao siku hiyo.
Kwa Upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Bw. Hashim
Mgandilwa ameelezea jitihada za usafi wa mazingira katika mji wa kigamboni
ikiwa ni pamoja na mashindano ya usafi wa mazingira na kuwataka wakazi wa kigamboni
kuongeza jitihada za kutosha kuiweka kigamboni safi.
Jumamosi ya Mwisho wa Mwezi ni siku maalum ya usafi ikiwa ni katika
kutekeleza agizo la Rais la Usafi wa mazingira ambapo mwezi huu kitaifa
imefanyika Kigamboni.
Naibu
waziri wa Nchi ofis ya makamu wa rais muungano na mazingira Mh.Luhaga Mpina
akifanya usafi na wananchi wa wilaya ya kigamboni katika kutekeleza agizo la Mh.
rais la kila mwisho wa mwezi kufanya usafi.
Naibu Waziri wa Nchi ofis ya Makamu
wa Rais Muungano na Mazingira Mh.Luhaga Mpina akiwa na wananchi wa kigamboni
waliojitokeza kwaajiri ya kufanya usafi katika fukwe za kigamboni
|
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...