Katika kuendeleza utendaji kazi kwa ufanisi kwa vituo vya Mafuta nchini ambao changamoto zake zimeonekana na gharama ambazo wanazotoa katika kutimiza huduma zinazotolewa na Halmashauri za jiji ambazo zimekuwa hazifidiwi kwenye bei inayoelekezwa na Ewura.

Kwa kuliona hilo Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa huduma za Nishati na Maji (EWURA) Felix Ngamlagosi ameitisha mkutano na wadau wa Mafuta ambapo lengo lilikuwa ni kujadili changamoto hizo.

Akizungumza mara baadaya kikao hicho Ngamlagosi amesema kuwa huduma zinazochangiwa ni muhimu kwani zinasaidia sana kuimarisha usalama mahali pakazi.

Aidha amesisitza kuwa tozo hizo zina umuhimu kwani husaidia pindi yanapotokea maafa kazini hasa moto na uhalali wa vipimo vya kupimia mafuta ili kuepusha wizi wa vipimo.

Kwa upande wake Malegesi Manyama ambaye ni muuzaji wa mafuta kwa rejareja yeye ameeleza kuwa Changamoto kubwa ni mtaji pamoja na upatikanaji wa mkopo katika kuendesha biashara hiyo hivyo michango hiyo huathiri gharama za mwendesha kituo.

 Mkurugenzi mtendaji wa Ewura, Felix Ngamlagosi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo alipokutana na wadau wa mafuta na kuzungumza nao.
Mdau wa kuuza Mafuta TAPSOA, Mahafudhi Maulid akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya wadau wa mafuta kuzungumza na Mkurugenzi mtendaji wa Ewura, Felix Ngamlagosi.
Wadau wa mafuta wakimsikiliza Mkurugenzi mtendaji wa Ewura, Felix Ngamlagosi jijini Dar es Salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...