JESHI la Polisi mkoa wa Mbeya linapenda kuwajulisha wananchi wote kuwa kutakuwa na uzinduzi wa majengo ya ofisi za dawati la jinsia na watoto zilizopo Polisi kati Mbeya na kituo kidogo cha Polisi ilomba, uzinduzi huu utafanyika tarehe 30.09.2016 Ijumaa.

Majengo hayo ya ofisi za dawati la jinsia na watoto ni moja kati ya majengo yanayojengwa nchi nzima katika kutekeleza mpango mkakati wa kujenga miundo mbinu ya ofisi za dawati la jinsia na watoto unaofadhiliowa na UNICEF.

Hivyo wananchi mjitokeze kwa wingi katika kushuhudia tukio hilo muhimu na la kihistoria katika mkoa wetu wa Mbeya.

Mgeni rasmi atakuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Amos Makala
kauli mbiu:- Funguka tumia dawati la jinsia na watoto kutokomeza ukatili wa kijinsia.
Imetolewa na.
Ofisi ya Kamanda wa Polisi
Mkoa wa Mbeya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...