Na MatukiodaimaBlog.
SERIKALI ya
mkoa wa Iringa
imepongeza msaada mkubwa uliotolewa na kampuni ya Asas
ya mkoa hapa wa ujenzi wa jengo
la kituo
cha damu salama
cha kisasa na ujenzi wa jengo la
watoto wanaozaliwa njiti katika
Hospitali teule ya mkoa
wa Iringa pamoja miradi itakayogharimu zaidi ya Tsh
milioni 400
Katika taarifa iliyosomwa na mganga mkuu
wa Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa Dr Robert salim wakati wa
hafla ya uwekaji wa jiwe la
msingi katika miradi hiyo leo mbele ya
mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza
alisema kuwa awali uongozi wa hospitali hiyo
ulimwandikia barua mfanyabiashara huyo
ili kusaidia msaada wa kontena ambalo lingetumika katika kituo cha benki ya damu salama ila mfanyabiashara huyo alijitolea kujenga jengo
hilo la kisasa na kuongeza msaada
wa jengo la watoto wanaozaliwa njiti .
“Kutokana na agizo la Serikali la
kuanzisha Benki za damu salama katika Mikoa..... Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa
kushirikiana na Mfadhili
Salim F. Abri Mkurugenzi wa Kampuni ya ASAS iliona ni vyema kujenga jengo la Kituo
Kidogo cha damu salama katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ili kufikia azma hiyo.
...Hospitali ilimuomba Mfadhili huyo atoe msaada wa “Container” kwa ajili ya
shughuli hiyo, lakini Mfadhili kwa kuona umuhimu wa huduma ya damu salama
katika Mkoa aliomba apewe ramani ili ajenge kituo hicho badala ya
kutumia“Container”.”alisema
Dr
Salim alisema kuwa Hospitali hiyo kabla ya mfanyabiashara huyo
kujitolea ujenzi wa jengo
hilo kituo cha kidogo
cha damu salama ulikuwa
ukitegemea damu kutoka
kituo cha kanda kilichopo
mkoani Mbeya ila
sasa wataweza kukusanya
damu kupitia kituo
hicho.
Alisema kuwa lengo la mradi huu ni Kuboresha upatikanaji
wa huduma za damu salama katika Mkoa wa Iringa kutokana na kuongezeka kwa
mahitaji ya damu salama katika Vituo vya kutolea huduma za afya na kupunguza
vifo vya Uzazi, Watoto wachanga, Watoto na Wahanga wa ajali za barabarani na
kuwa lengo la Mkoa kwa mwezi ni kukusanya chupa 784 na kwa mwaka ni chupa 9,413
(units).
Hata
hivyo alisema mahitaji ya damu
kwa mwezi katika Mkoa ni chupa 700 (unit) na katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa
ni chupa 160-200 Units kwa mwezi kuwa tangu kituo kianze kutumika mwezi
Februari,2016 Mkoa umekusanya chupa 2,065 (22%) hadi sasa.
“Tunakushukuru mkuu wa mkoa kwa kukubali mwaliko wetu wa kuwa Mgeni Rasmi katika
hafla hii ya kuweka mawe ya msingi katika miradi ya maendeleo inayotekelezwa na
Mfadhili wetu Salim F. Abri Mkurugenzi wa Kampuni ya ASAS ya Iringa. Katika
hafla hii fupi tutakuomba uweke jiwe la Msingi katika Mradi wa jengo la Kituo
Kidogo cha Damu Salama na Jengo la Wodi ya Watoto wachanga vyote vikiwa ni
hisani kutoka kwa mfadhili
wetu Salim F Abri “
Alisema
kuwa ujenzi huo unafanywa namkandarasi anayenga mradi huu
ni Buyungu General Enterprise wa Iringa chini ya usimamizi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ambaye
amechangia kuchora ramani za jengo hili na kusimamia mradi mpaka ulipokamilika,
mchango wake kama angelipwa ni Tshs.13,939,200.00.
Na
kuwa utekelezaji wa mradi ulianza kutekelezwa
mwezi Novemba, 2014 na umekamilika mwezi Agosti, 2015. Jengo limeanza kutumika
mwezi Februari, 2016. Pamoja na kujenga jengo hili Mfadhili pia ametoa msaada
wa samani, mafriji makubwa 4 ya kutunzia damu na Computer 1 wenye thamani ya
Tshs.30,000,000.00.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...