TAMASHA la Kandanda maarufu kama ‘Kandanda Day’, linatarajia kufanyika Oktoba 15,  mwaka huu katika kiwanja cha Jakaya Kikwete Park (zamani Kidongo Chekundu).

Katika tamasha la mwaka huu,kauli mbiu itakuwa ni ‘Mpira na Dawati’ ikiwa na lengo la kukusanya fedha kwa ajili ya kununua madawati yatakayogawiwa kwa shule mbalimbali nchini.

Mratibu wa tamasha hilo,Mohamed Mkangara,amesema kwamba mwaka huu wameamua kuja na kauli mbiu hiyo, ili kuunga mkono kampeni inayoendelea ya Serikali kuhusu madawati kwa shule za msingi na sekondari.
 “Umekuwa ni utaratibu wetu kila mwaka huu,kuja na kauli mbiu ambayo itahusisha soka na jambo ambalo moja kwa moja linaihusu jamii,kwahiyo, tumeona kwa kutumia soka,tunaweza kuisaidia jamii yetu kwa urahisi,”amesema  Mkangara

“Ndio maana kwa miaka yote tuliyofanya tamasha letu,kumekuwepo na ‘impact’ ya moja kwa moja kwa jamii inayotuzunguka,kwa hiyo ule utamaduni wetu tuliokuwa nao kwa miaka minne tunaendelea nao kwa mwaka huu kwa kukusanya fedha kwa ajili ya manunuzi ya madawati,ambapo tunatarajia kuchangisha fedha na kuuza jezi katika ‘dinner’ maalum ambayo tumeandaa kwa wadau mbalimbali.”
Mkangara,amesema kwamba madawati ambayo yatapatikana yatagawiwa kwa wawakilishi waliochaguliwa wa Kandanda kutoka mikoa mbalimbali nchini, ambao watahudhuria siku hiyo.

Tamasha la mwaka huu linatarajia kushirikisha timu mbalimbali alikwa,ukiacha timu wenyeji Time Dizo Moja na Timu Ismail.Pia,tamasha hilo linatarajiwa kupambwa na burudani mbalimbali na michezo ya kuvuta kamba kwa washiriki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...