Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mheshimiwa Nape Nnauye ametoa ofa kwa
wananchi kujumuika pamoja leo Septemba 18, 2016 katika mchezo wa mpira wa miguu
utakaozikutanisha timu za vijana taifa za Tanzania na Congo-Brazzaville kwenye
Uwanja wa Taifa, ulioko Chang’ombe, jijini Dar es Salaam.
Timu hizo
zitakutana kweye mchezo wa kwanza kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la
Mataifa ya Afrika kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka. Zinatarajiwa
kurudiana Oktoba 2, 2016 huko Congo Brazzaville na timu itafayopata ushindi wa
jumla katika michezo miwili itafuzu kwa fainali hizo.
Nape alitoa ofa hiyo tangu jana Septemba 17, 2016 na leo asubuhi
Septemba alipata kifungua kinywa na wachezaji wa Serengeti Boys ambako alitoa
Sh 200,000 kwa kila mchezaji zilizotokana na kundi linalosapoti Serengeti Boys
ambao walichangia Sh 2,600,000 wakati nyingine zilitoka kwa wadau wengine.
Nape ameahidi pia kununua bao moja kwa Sh 500,000 na atalipa
fedha hizo kadiri ya idadi ya mabao hata kama yatafika 10 hivyo gharama yake
itakuwa Sh 5,000,000. “Kuna wabunge na viongozi wengine wameahidi kutoa fedha
zaidi, kwa hiyo Serengeti Boys kazi kwenu kutafuta ushindi leo mbele ya
Watanzania watakaoingia uwanjani bure.”
Kuingia bure kesho ni ofa iliyotolewa na Nape ambako Rais Jamal
Malinzi amemshukuru Nnauye ambaye ni Mbunge wa Mtama kwa ofa hiyo ambayo
imelenga kutoa hamasa kwa Watanzania kwenda kushangilia timu yao.
Katika mchezo huo ambao Kocha
Mkuu wa Serengeti Boys, amesema kwamba amemaliza kila kitu na kwamba anasubiri
Watanzania kuja uwanjani leo kuishangilia timu yao, utachezwa na waamuzi kutoka
Shelisheli ambako mpiga kipenga atakuwa Nelson Fred akisaidiwa na Hensley
Petrousse na Stive Marie wakati mwamuzi wa akiba akiwa Allister Barra. Kamishna
wa mchezo atakuwa Gladmore Muzambi kutoka Zimbawe.
|
Home
Unlabelled
KUONA SERENGETI BOYS NA CONGO BRAZZAVILLE LEO BURE, VIJANA WAJAZWA NOTI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...