Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
BODI ya Ligi kupitia Shirikisho La Mpira wa Miguu Nchini TFF, limetangaza mabadiliko ya ratiba ya ligi na kutangaza tarehe ya mchezo namba 1 wa kiporo baina ya Mabingwa wa Ligi Kuu Vodacom Yanga na JKT Ruvu.

Mchezo huo iliokuwa wa ufunguzi wa ligi ulishindikana kuchezwa Agosti 21 baada ya Yanga kuwa na mchezo wa kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya TP Mazembe Nchini Kongo.

Bodi ya ligi imeupeleka mchezo huo hadi Oktoba 26 ambapo ahapo awali walisema kuwa watatangaza ni lini utachezwa, na katika hilo  mchezo namba 57 baina ya Mwadui na Azam, mchezo namba 60 TZ Prisons na Simba utachezwa Novemba 09, mchezo namba 59 Yanga na Ruvu Shooting utapigwa Novemba 10.

Mchezo namba 69, Yanga na Mtibwa utachezwa Oktoba 13, mchezo namba 97 Kagera na Azam utapigwa Oktoba 28 na katika mchezo namba 100 baina ya Yanga na Mbao , namba 102 Toto na Mtibwa Sugar  utapigwa Oktoba 30, Mtibwa na Mbeya City mchezo namba 113 na namba 115 kati ya Mwadui na Majimaji zote zitapigwa Novemba 07.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...