Na Chalila Kibuda, Globu ya jamii

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa upandaji miti Mkoa wa Dar es Salaam.

Akizungumza leo na waandishi wa habari ofisini kwake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema upandaji wa miti unaanza kesho hivyo kila mwananchi wa Dar es Salaam anatakiwa kupanda mti mmoja ikiwa ni kwa ajili ya ustawi wa afya.

Amesema kuwa upandaji miti utafanywa katika Wilaya yaTemeke kwa kupanda miti katika barabara ya Kilwa na baada kupanda miti atakagua miundombinu ya maji kwa ajili ya kumwagilia miti katika Wilaya Ilala pamoja na Kinondoni.

Makonda amesema miti hiyo itakayopandwa ni faida ya Mkoa wa Dar es Salaam kwa ajili hewa na pamoja na vivuli vya kupumzika.Aidha amesema kila mwananchi lazima afanye jitihada za kupanda miti ikiwa ni pamoja watendaji wote wa mitaa na kata kuhamasisha wananchi kupanda miti.

Hata hivyo amewataka mashabiki wa yanga na simba kupanda miti kabla ya kuanza mpira kati timu hizo.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza leo na waandishi habari juu ya upandaji miti utaozinduliwa kesho,jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka Globu ya Jamii)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...