Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akimkabidhi fedha taslimu Shilingi 1,119,000, Msimamizi wa Kituo cha Watoto Yatima cha Moyo wa Huruma kilichopo mjini Geita, Sista Adalbera Mukure kwa ajili ya kusaidia majukumu mbalimbali ya ulezi wa watoto hao. Fedha hizo zilitolewa na Masauni pamoja na Wajumbe wa Baraza hilo kwa lengo la kusaidia kituo hicho. Pia Baraza hilo lilitoa mchele gunia moja, kilo 50 za sukari, dumu la mafupta ya kupikia, sabuni Katoni 11 pamoja na fulana 100.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (aliyembeba mtoto) na Katibu wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga (kulia) wakiwa na baadhi ya watoto Yatima wa Kituo cha Moyo wa Huruma cha mjini Geita, mara baada ya Masauni kukabidhi fedha taslimu shilingi 1,119,000 pamoja na vyakula kwa kituo hicho ambapo misaada hiyo ilitolewa na Baraza la Usalama barabarani ambalo linaadhimisha Wiki ya Nenda kwa Usalama mjini humo.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa
la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (aliyembeba mtoto), Mkuu wa Mkoa
wa Geita, Meja Jenerali Mstaafu, Ezekiel Kyunga (kulia kwa Masauni), pamoja na Wajumbe wa Baraza la Taifa la
Usalama Barabarani wakiwa katika picha ya pamoja na Watoto Yatima wa Kituo cha
Moyo wa Huruma cha mjini Geita, wakati Mwenyekiti huyo wa Baraza pamoja na
wajumbe wake kukitembelea kituo hicho na kukabidhi misaada mbalimbali. Tukio
hilo lilifanyika mara baada ya Masauni kuizindua Wiki ya Nenda kwa Usalama
Barabarani ambayo inaadhimishwa Kitaifa mjini Geita. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...