Daraja la Makutopora linalounganisha
Wilaya ya Chemba na Manyoni likiwa limekamilika kujengwa, daraja hilo
limejengwa kwa gharama ya shilingi milioni 628,247,000 na kisha
kuzinduliwa na kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru George Jackson
Mbijima. Mbijima amewaasa wananchi wa wilaya zinazounganishwa na daraja
hilo kutumia fursa ya uwepo wa barabara na miundombinu mizuri katika
kuboresha maendeleo yao.
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru
George Jackson Mbijima akipita katika daraja la Makutopora
linalounganisha Wilaya ya Chemba na Manyoni likiwa limekalika kujengwa,
daraja hilo limejengwa kwa gharama ya shilingi milioni 628,247,000
kutoka serikali kuu na kisha kuzinduliwa na kiongozi wa mbio za mwenge
wa uhuru George Jackson Mbijima.
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru
George Jackson Mbijima akizungumza na wanafunzi na wananchi
waliojitokeza katika uzinduzi wa madarasa mawili na matundu ya vyoo nane
katika sekondari ya Chikuyu yenye thamani ya shilingi milioni 108,
448,49.
Afisa wa mradi akitoa maelezo ya mradi
wa ufuatiliaji naudhibiti wa mbu waenezao malaria, huku gharama ya
mradi huo ikiwa ni shilingi milioni sita na nusu.
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru
George Jackson Mbijima akizungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza
kushuhudia uzinduzi wa kituo cha maarifa ya kupambana na ukimwi chenye
thamani ya shilingi 87,584, 007. Mbijima amewaasa wakazi wa Manyoni
kukitumia kituo hicho ili kiwasaidie katika mapambano dhidi ya Ukimwi.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...