Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 
WANAFUNZI 2548  katika shule za Sekondari na Msingi 12 wamebainika  kuwa hewa katika Manispaa ya Temeke.

Akizungumza na Wakuu wa Shule wa Sekondari, Msingi, Waratibu wa tarafa na Kata, Mkuu Wilaya ya Temeke, Felix Lyaviva amesema wanafunzi hao wamechukua fedha nyingi pamoja na kuhangikia madawati.

Lyaviva amesema kuwa walimu wakuu katika shule zilizobaki wanatakiwa kuhakiki wanafunzi katika kuweza kuondokana na wanafunzi hewa katika kuweza kupanga bajeti vizuri.

Amesema kuwa wanafunzi hewa wa kwa shule za msingi 1986 na Shule za Sekondari 859 ambao wanafunzi hao walikuwemo katika madawati na kufanya nguvu zaidi kutumika kwa wanafunzi hewa hao.
Mkuu wa Wilaya Lyaviva amesema walimu waliohusika katika kufanya hivyo watachukuliwa hatua ikiwa ni kutaka wafanyakazi kufanya kazi kwa utaratibu.
Aidha amewataka wakuu wa shule kuwa na utaratibu wa kuhakiki wanafunzi ili kuweza serikali kupanga bajeti ambayo inaenda kufanya kazi iliyokusudiwa na sio bajeti kwenda kwa wanafunzi hewa 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...