Na. Aron Msigwa – NEC, Musoma

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeanza kutekeleza programu endelevu za kutoa elimu ya mpiga kura ili kuwaelimisha wananchi waliofikisha umri wa kupiga kura kutekeleza wajibu na haki waliyonayo kikatiba ya kupiga kura katika chaguzi zijazo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani wakati akizungumza na waandishi wa Habari mjini Musoma kuhusu mkakati wa NEC wa kuwafikia wananchi moja kwa moja kuwapatia elimu ya mpiga kura.

Amesema kuwa Tume hiyo imeanza kutoa elimu hiyo kwa kushiriki maonesho na mikutano mbalimbali ukiwemo mkutano wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) unaofanyika mjini Musoma kuanzia Septemba 22 hadi 24 mwaka huu.

“Tumeamua kushiriki kwenye mkutano huu kwa kuwa hawa ni watendaji wa Serikali katika ngazi za mitaa, tumekuja kutoa elimu ya mpigakura kwani suala la elimu tunalipa kipaumbele” Amesema Bw. Kailima.

Amesema Tume imeandaa programu ya kuwafikia wapiga kura moja kwa moja kwa kuweka mkakati wa kuhudhuria mikutano yote ambayo iko kihalali ikijumuisha ile ya Mawaziri na Naibu Mawaziri , Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya.

Amebainisha kuwa tayari NEC imewasiliana na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ili iweze kupata ratiba ya vikao vya kamati za ushauri za mikoa na wilaya ili iweze kupata fursa ya kutoa elimu ya mpiga kura ndani ya vikao hivyo.

Aidha, amefafanua kuwa Tume imemwomba Katibu Mkuu TAMISEMI ratiba ya vikao vya Mabaraza ya madiwani ya halmashauri zote nchini kwa lengo la kuwezesha wataalam wa Tume hiyo kutoa elimu ya Mpiga kura.

“Tumemwomba Katibu Mkuu TAMISEMI atusaidie kuweka ajenda ya kudumu kuhusu utaratibu mzima wa uendeshaji wa uchaguzi na uelimishaji wa mpiga kura kwenye vikao vya mabaraza ya Madiwani ambapo maafisa wa Tume walio katika ngazi za halmashauri watapata fursa ya kutoa elimu ya mpiga kura katika vikao hivyo” Amesisitiza.



Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani akizungumza na waandishi wa Habari mjini Musoma kuwaeleza mkakati wa NEC wa kuwafikia wananchi moja kwa moja kuwapatia elimu ya mpiga kura.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...