Na Mwandishi Maalum, New  York

Ufalme wa Oman umeonesha nia ya  kukarabati  majengo  ya makubusho ya kale   ya  Beit Al Jaib  maarufu kama “ House  of  Wonders” yaliyopo  mjini  Unguja – Zanzibar.

Nia hiyo imeoneshwa na   Waziri wa Mambo ya   Nje wa  Oman,  Bw. Yusuf bin Alawi bin Addullah wakati   alipokutana na kufanya  mazugumzo na  Waziri wa Mambo ya Nje  na  Ushirikiano wa  Afrika Mashariki, Dkt, Augustine Mahiga.

Mazungumzo  baina ya  viongozi  hao wawili  yalifanyika  pembezoni mwa  Mkutano wa 71 wa  Baraza Kuu la  Umoja wa Mataifa, ambapo  Mawaziri hao walikuwa wakiongoza ujumbe wa Nchi  zao.

Mazungumzo   ya   Mawaziri  hao  yalijikita  katika   uimarishwaji wa uhusiano  na ushirikiano mzuri  uliopo  baina ya  Oman na  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 Katika majadilaino hayo ambapo   pamoja  na  mambo mengine,  Waziri  Mahinga  aliomba  serikali ya Oman kuangalia uwezekano  wa kuanzishwa  kwa miradi wa kutunza mambo ya kale zikiwamo nyaraka muhimu zinazohusu uhusiano  baina ya nchi  hizo mbili.

Waziri Mahiga  alieelezea  pia hali uchakavu wa  majengo ya   Beit Al Jaib ( House of wonders)   majengo yaliyokuwa  Ikulu ya  utawala wa Kifalme, Zanzibar.  Makubusho hayo  yamesheheni historia ya  uhusiano  na ushirikiano kati  ya  Zanzibar na   Sultanate of Oman na  Afrika  Mashariki kwa Ujumla.

Na kutokana na historia hiyo na  umuhimu wa  jengo hilo ambalo limejengwa mwaka 1883, Waziri ameiomba  Serikali ya  Oman kuangalia  uwezekano wa kulihifadhi jingo hilo ambalo pia ni kivutio kikubwa cha utalii.

Akijibu  ombi  hilo na  mengine yaliyowasilishwa na   Waziri Mahinga,  Waziria wa Mambo ya Nje wa Oman,  Bw .   Yusuf bin Alawi bin Addullah amemtaka  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa  Afrika   Mashariki kuandaa andiko  na  kuliwasilisha  katika Serikali ya  Oman ili  pendekezo  hilo liweze  kufanyiwa kazi pamoja na mapendekezo mengine.

Katika  hatua nyingine,  Waziri wa Mambo ya Nje  na  Ushirikiano wa   Afrika Mashariki,  Augustine  Mahiga amekuwa na   kuwa  na mazungumgo na   Bi. Linda Thomas Greenfield,   Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayehusika na  masuala ya   Afrika.

Mazungumzo ya  Waziri Mahinga na   Bi.  Linda Greenfield yalijikita zaidi  katika uhusiano na  ushirikiano  baina ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Marekani.
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sultanate of Oman, Dkt Augustine Mahiga ( kushoto) na Yusuf bin Alawi bin Abdullah wakizungumzia kuhusu namna ya kuendelea kuimarisha uhusiano mzuri baina ya nchi hizo mbili. Katika mazungumzo hayo Waziri Mahiga ameiomba serikali ya Oman kupitia Waziri Abdullah kuangalia uwezekano wa kushirikiana katika uhifadhi ya nyaraka na kumbukumbu muhimu pamoja na ukarabati ya jengo la House of Wonders lilojengwa na ufalma wa Oman mwaka 1883.
Jengo maarufu la Beit Al Jaib ( House of Wonders) ambalo Serikali ya Tanzania inaiomba Serikali ya Oman kuangalia uwezekano wa kulikarabati kama sehemu ya mradi wa kuhifadhi nyaraka, kumbukumbu na majengoa ya kihistoria visiwani Zanzibar
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mshariki, Augustine Mahiga akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayehusika na masuala ya Afrika, Mazungumzo yao yalijielekeza zaidi katika uhusiano na ushirikiano kati ya nchi hizi mbili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. I cant imagine Zanzibar without Bei al Ajeib
    Jengo hili likianguka ama likibomolewa itakuwa ni hasara kubwa sana kwa historia ya Zanzibar.Beit al Ajeib has Zanzibar written all over it. Niliwahi kuona mtalii mmoja akijitapa kuwa ameshafika Zanzibar na to prove it he was showing off his selfie infront of the building.

    ReplyDelete
  2. Good initiative from our beloved Omani government, we ask Allah almighty to give long life HM Sultan Qaboos alhamdulillah

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...