Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amekagua
athari za tetemeko la ardhi lililoikumba miundombinu ya barabara katika mkoa wa
Kagera na kujionea athari zilizojitokeza katika mkoa huo.
Prof. Mbarawa amejionea athari za tetemeko la ardhi katika barabara ya Rwamishenye
hadi Bandari ya Bukoba yenye urefu wa KM 4.6 ambayo imeathirika mita 60 na
barabara ya Bukoba-Mtukula yenye urefu wa KM 80 ambayo imeathirika kwa mita 200
na kusisitiza kwamba Wizara yake itatekeleza maelekezo yaliyotolewa na Waziri Mkuu
Mhe. Kassim Majaliwa ili kukabiliana na changamoto zilizojitokeza.
“Tunatoa pole kwa wananchi wa mkoa wa Kagera kutokana na maafa yaliyojitokeza
hivyo tutafanyia kazi maelekezo ya ukarabarati wa miundombinu iliyoathiriwa na
tetemeko kadiri tulivyoelekezwa na Waziri Mkuu”, amesema Prof. Mbarawa.
Prof. Mbarawa yuko mkoani Kagera kukagua athari za uharibifu wa miundombinu
kufuatia tetemeko la ardhi lililopiga mikoa ya Kagera, Mara na Mwanza Septemba 10
mwaka huu na kusababisha vifo vya watu takribani 16, majeruhi zaidi ya 100,
uharibibifu wa nyumba takribani 800 na miundombinu.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa
maelekezo kwa mafundi wa wanaodhibiti eneo lililoathirika na tetemeko la ardhi katika
barabara ya Bukoba-Mtukula yenye urefu wa KM 80 ambayo imeathirika kwa mita 200,
mkoani Kagera.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizungumza
na Meneja wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), mkoa wa Kagera Eng.
Andrea Kasamwa wakati alipokagua athari za tetemeko la ardhi lililoikumba
miundombinu ya barabara mkoani humo.
Muonekano wa sehemu ya barabara ya Rwamishenye hadi Bandari ya Bukoba yenye
urefu wa KM 4.6 ambayo imeathirika mita 60 kutokana na tetemeko la ardhi mkoani
Kagera.
Huyo waziri ni jembe !! Hongera Na piga kazi. Wengine wapo maofisini Na viyoyozi Na viti vya kuzunguka Ila wewe upo uwanjanj penye kutekeleza kazi !!!!
ReplyDelete