Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Puma Energy Tanzania,Phillipe Corsaletti akimkabidhi stika Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,Kamanda Mohamed Mpinga ,zitakazotumika katika zoezi la ukaguzi wa magari katika juma la wiki ya usalama barabarani,inayotarajiwa kuanza hivi Karibuni.Bwa.Phillipe alisema kuwa hiyo ni sehemu ya uwekezaji wao katika masuala ya usalama barabarani ambao wanaamini ni wa muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa."Tunaamini kuwa shughuli zetu zinaweza tu kuwa salama kama jamii inayotuzunguka ipo salama",alisisitiza Mkurugenzi huyo.
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Puma Energy Tanzania,Phillipe Corsaletti pamoja na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,Kamanda Mohamed Mpinga wakionesha baadhi ya stika mbele ya mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika mapema leo katika ofisi za makao makuu ya Trafiki,jijini Dar Es salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Puma Energy Tanzania,Phillipe Corsaletti akisoma taarifa yake kabla ya kukabidhi stika za Usalama Barabarani kwa Jeshi la Polisi Kitengo cha usalama Barabarani ,mbele ya mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika mapema leo jijini Dar.Bwa.Phillipe alieleza kuwa suala la usalama barabarani linaendelea kuwa na changamoto kubwa duniani kote,amesema kuwa kwa hapa Tanzania jamii inashuhudia ajali za barabarani karibu kila siku.

"Ajali hizi zinawagusa vijana na wazee,wanataaluma,wafanyabiashara,wakulima,wanasiasa,matokeo ya ajali hizi ni vifo,majeruhi,uharibifu wa mali,upotevu wa wataalamu na mwisho kabisa mzigo mkubwa ni kwa Taifa",alifafanua Bwa,Phillipe.

Hivyo Bwa,Phillipe ameziomba mamlaka zinazohusika kuyatazama mambo hayo kwa undani na kuweka mfumo ambao utasaidia kuondoa ama kupunguza kwa kiaisi kikubwa wimbi la ajali za barabarani.Mkurugenzi huyo amesema kuwa pamoja na kuwa na wadau wakubwa wa mambo ya usalama barabarani pia wamekuwa wakitoa elimu kwenye shule mbalimbali za msingi hapa nchini na kuwa mpaka sasa wamefanikiwa kuzikifia shulu 30,amesema na kuongeza kuwa lengo lao kubwa ni kuzifikia shule zote za msingi za serikali hapa nchini kupitia mpango huo wa kutoa elimu ya usalama barabarani kwa shule za msingi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...