NA NTEGHENJWA
HOSSEAH - ARUSHA.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka
Gambo amewafuta machozi wananchi wa mtaa wa Mlimani kwa mama hadija kwa
kumaliza mgogoro uliodumu muda mrefu ambao ulilenga kubomoa nyumba zaidi ya 127
za makazi na biashara kwa wananchi wa eneo hilo ili kupisha mradi mkubwa wa
maji uliopangwa kutekelezwa na Idara ya mji safi na maji taka (AUWSA).
Uamuzi huo ulitoka kwenye bodi ya maji ya
AUWSA ambayo miongoni mwa wajumbe wake ni Meya wa Jiji, Mkurugenzi pamoja na Katibu
tawala Mkoa wa Arusha kupitia vikao vyao vya kisheria walipitisha maamuzi ya
kuweka X kwenye nyumba hizo kwa nia njema ya kutekeleza mradi mkubwa wa maji
ambayo ungewasaidia wananchi wa eneo la kwa mrombo na Murieti kuondokana kabisa
na changamoto kubwa ya maji waliyonayo.
Kitendo hicho chenye nia njema kililtea
tafrani na sinfofahamu kwa wananchi waliojenga nyumba kwenye maeneo hayo.
Kupitia kilio hicho cha wananchi Serikali ya Mkoa iliyapitia kwa kina malalamiko
hayo na kutoa Tamko la Serikali la kuwataka Mamlaka zinazohusika yaani Jiji la
Arusha na Mamlaka ya Maji kusitisha mara moja zoezi la bomoa bomoa na kuwataka
watafute chanzo kingine cha maji ili wananchi waweze kupata maji kama Serikali
ilivyokusudia.
Akizungumza na hadhara hiyo Mkuu wa Mkoa Mhe Gambo alisema zoezi la bomoa bomoa lililokuwa lifanyike katika
eneo hili limesitishwa si kwa sababu hakuna Maji katika eneo hilo lakini tumethamini
jasho lenu na nguvu mlizotumia kujenga nyumba hizi hivyo kwa maslahi mapana ya
wananchi wetu haswa wanyonge tumeona tuliondoe eneo hili kwenye orodha ya
maeneo yaliyokua yatumike kuchimba visima vya AUWSA na kwa ajili yenu
tumelibakiza kwa ajili ya makazi halali na tutangalia namna nyingine ya
kuwapatia maji safi ila sio kwa kubomoa hizi nyumba zenu hivyo kuanzia sasa alama za X zilizowekwa kwenye nyumba zenu zisiwazuie
kuendelea na shughuli zenu za kuendeleza maeneo yenu na kuishi kwa mani.
Aidha alimuelekekeza Mkurugenzi wa Jiji
kumuandikia barua Mtendaji wa Kata na Mtaa unaohusika ili kuwajulisha wananchi
hao kwa maandishi kwamba Serikali imesitisha zoezi la bomoa bomoa na wananchi
wabaki huru kwenye maeneo yao.
Akitao Shukrani kwa Serikali Ndg. Iddi Ally
Hindi alisema hawaamini kwamba suala hili limepatiwa ufumbuzi maana mgogoro huu
umedumu kwa muda mrefu na muda wote huo wamekua wakiishi kwa mashaka kwenye
nyumba zao kutokana na alama za X zilizowekwa zikimaanisha kwamba siku yeyeote
nyumba hizo zingebomolewa hivyo walisubiria lolote kutokea lakini kwa kauli hii
kutoka Mkuu wa Mkoa imewatia faraja na sasa wataishi kwa amani.
Aidha wananchi walitoa malalamiko yako kwa
Viongozi wa Serikali kwamba wanaomba kujengewa Zahanti kwa kuwa hivi sasa
wanatembea umbali mrefu kufuata huduma za Afya na aliyekuwa mmiliki wa eneo
hilo Bi. Thedy James maarufu kama Mama hadija alitoa eneo la nusu heka kwa Serikali ili iweze kujenga Zahanati kwa wateja wake aliowauzia
maeneo hayo ambapo kwa sasa wakazi wa eneo hilo ni zaidi ya elf elfu mbili.
Mkuu wa Mkoa
Mhe. Gambo alimshukuru Bi. Thedy kwa kutoa eneo hilo pia alimuagiza Mkurugenzi
wa Jiji kutuma wataalamu kwenda kuangalia eneo na kuanza maandalizi ya awali
kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati hiyo.
Viongozi
walioshiriki kwenye Mkutano na wananchi wa mtaa wa Kilimani kwa Mama Hadija,
Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi wa Jiji Ndg. Athumani Kihamia, Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Gabriel
Daqarro, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo, Mwenyekiti wa Bodi
ya AUWSA Dr. Laiza pamoja na Mkurugenzi wa AUWSA Eng Ruth Koya .
Mkuu
wa Wilaya ya Arusha Mhe. Fabian Daqarro (aliyesimama) akimkaribisha Mkuu wa
Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo kutoa tamko la Serikali kwa wananchi wa mtaa
wa Mlimani kwa Mama Hadija
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo (aliyesimama) akiongea na wananchi wa mtaa wa Kilimani kwa mama hadija kuhusu hatma ya nyumba zao zilizokuwa zibomolewe kupisha mradi wa maji. |
Nyumba
hii pia ni miongoni mwa nyumba zilozokuwa zimewekwa X kupisha Mradi wa maji uliokuwa utekelezwe
katika eneo hilo.
|
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...