Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Amina Masenza akizungumza katika Ufunguzi wa Mafunzo ya siku moja ya kuwajengea uwezo Wakurugenzi na Wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wake kuhusu kusimamia kikamilifu Mpango mpya wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa bila ya malipo Kwa watoto wenye Umri chini ya miaka mitano katika Mkutano uliofanyika katika ukumbi wa VETA Mjini Iringa, ambapo utekelezaji wake utaanza hivi karibuni katika Mikoa ya Iringa na Njombe. kulia kwake ni Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA, Bi. Emmy Hudson, anayemfuatia kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Mhe. Richard Kasesela na Mwingine ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa huo, Bw. Nuhu Mwasumilwe.
Wajumbe wa mkutano wakifuatilia Hotuba ya ufunguzi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Amina Masenza kuhusu usimamizi na ufuatiliaji wa Mpango mpya wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa bila ya malipo Kwa watoto wenye Umri chini ya miaka mitano pindi utakapoanza kutekelezwa katika Halmashauri na Wilaya zote za Mkoa wa Iringa.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Amina Masenza akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wengine wa Mkoa, Wilaya na Halmashauri za Iringa, Kilolo na Mufindi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...