Mkuu wa Mkoa wa Geita, Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyuga (katikati) na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Bw.Frank Kanyusi (kulia) na washiriki wengine wakisikiliza mada ya Naibu Msajili – Sheria za Biashara(BRELA) Bw. Andrew Mkapa katika semina elekezi kwa wafanyabiashara mkoani humo juu ya umuhimu wa kurasimisha biashara na majukumu ya BRELA. Pia kuna usajili majina ya biashara na makampuni wa papo kwa papo kwa muda wa wiki nzima.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni na Biashara (BRELA), Bw.Frank Kanyusi katika hali ya furahana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyuga mara baada ya kufungua semina elekezi kwa wafanyabiashara wa mkoa huo juu ya umuhimu wa kurasimisha biashara zao. Pia kuna usajili majina ya biashara na makampuni wa papo kwa papo kwa muda wa wiki nzima.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...