Na: Frank Shija, MAELEZO
SERIKALI imewataka walimu wa shule za msingi na sekondari nchini kuwasilisha madai
yao yasiyo kuwa ya Mishahara ikiwemo stahili za likizo ili waweze kulipwa madai hayo
kwa wakati.
Hayo yamesemwa jana na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce
Ndalichako wakati wa mahojiano ya kipindi maalum cha TUNATEKELEZA
kinachorushwa na kituo cha Televisheni cha Taifa (TBC1).
Profesa Ndalichako alisema kuwa Madeni ya Walimu yamegawanyika katika sehemu
mbili ambazo ni madai yatokanayo na mishahara na yasiyokuwa ya mishahara ambayo
yamekuwa yakilipwa na Serikali kupitia Wizara yake ambapo hadi hivi sasa hakuna
mtumishi ambaye hajalipwa.
“Hakuna jalada la madai ya walimu yasiyokuwa ya mishahara na kama yapo madai
walete ili walipwe kwani fedha zipo”. Alisema Profesa Ndalichako na kuongeza kuwa
madai ya mishahara yamekuwa yakishughulikiwa na Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma ambapo nayo yamekuwa yakifanyika.
Kwa mujibu wa Profesa ndalichako alisema Serikali imekuwa ikipata ufadhili kutoka
Serikali ya Sweden kwa ajili ya kusaidia katika kulipa stahili mbalimbali za walimu ili
kuboresha weledi wa taaluma yao.
Kwa upande wa ubora wa Elimu, Ndalichako alisema kuwa pamoja na changamoto
zilizopo katika sekta elimu, ubora wa Elimu ya Tanzania umekuwa ukifanyiwa kazi
kupitia program mbalimbali zikiwemo za mpango wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu
(KKK).
Akitolea mfano Waziri Ndalichako alisema kuwa kumekuwapo na maboresho makubwa
tokea enzi za mpango wa UPE miaka ya 1970 ambao lengo lake lilikuwa kuwawezesha
wanafunzi wengi zaidi kujiunga na elimu ya msingi.
Waziri Ndalichako mwaka 2013 Serikali iliendelea kufanya maboresho kwa kuongeza
sifa za kujiunga na vyuo vya ualimu ili kupata walimu wenye ubora ndipo udahili wa
ikiwemo ufaulu wa daraja la tatu kwa wahitimu wa kidato cha nne na ufaulu wa
masomo mawili katika kidato cha sita.
“Serikali ilianzisha Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 ambayo ilibainisha kuwa
elimu ya msingi na mafunzo mwanafunzi atatakiwa atasoma darasa la kwanza hadi la
6 kwa msingi na mafunzo ni kuanzia darasa la 7 hadi la 12”.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...