Baadhi ya
wachezaji wa Timu ya Taifa ya Vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 -
Serengeti Boys, wakiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Maya Maya mara baada ya
kutua leo wakitokea Kigali nchini Rwanda walikopiga kambi kabla ya kuwavaa
vijana wenzao wa Congo Brazaville Jumapili ya Oktoba 2, 2016 kwenye dimba la Massamba
Sebat, Brazzaville. Timu hiyo imefikia
Hoteli ya Michael’s iliyopo Barabara ya Nelson Mandela jijini humo. Kikosi
hicho kimetua salama salmin kujindaa kuifumua Congo Jumapili. (Picha na Alfred
Lucas wa TFF).
Kutoa
kushoto, Kibwana Shomari, Yohana Mkomola na Rashid Ada wa Timu ya Taifa ya
Vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 - Serengeti Boys wakiwa Uwanja wa Ndege
wa Kimataifa wa Maya Maya mara baada ya kutua leo wakitokea Kigali nchini
Rwanda.
Wakiingia
Hotelini.
Serengeti Boys wakiingia Hotelini.
Makocha wa
Timu ya Taifa ya Vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 - Serengeti Boys,
Muharami Mohammed Sultan maarufu kama Shilton (kushoto) anayewanoa makipa,
Kocha Mkuu Bakari Nyundo Shime au Mchawi Mweusi na Mshauri wa Maendeleo ya soka
la Vijana, Kim Poulsen wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kuwasili Hoteli
ya Michael’s iliyopo Barabara ya Nelson Mandela jijini Brazzaville, Congo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...