Mkurugenzi wa Taasisi ya Ocean Road,  Dk. Julius Mwaiselage akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Kuhusiana na kupimepitisha muongozo wa tiba shufaa kwa wagonjwa waliokata tamaa katika hospitali za hapa nchini.
Baadhi ya waandishi wa jamii wakimsikiliza Mkurugenzi wa Taasisi ya Ocean Road,  Dk. Julius Mwaiselage jijini Dar es Salaam leo.

Na Yassir Adamu, Globu ya Jamii.
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya Maendeleo Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee imepitisha muongozo wa tiba shufaa (Tiba kwa wagonjwa walio kata tamaa) ili kuweza kutumika kwa wagonjwa mbalimbali.

Akizungumza na waandishi wa habari, leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Taasisi ya Ocean Road,  Dk. Julius Mwaiselage  amesema kuwa kuna umuhimu kwa kila hospitali za serikali na Binafsi kuwa na utoaji wa tiba shufaa.(Tiba kwa wagonjwa walio kata tamaa)

Amesema kuwa shufaa  inatumika kwa wagonjwa wa muda mrefu ambao wamekata tamaa katika kuondoa maumivu makali kuliko huduma nyingine kwa wagonjwa.

Dk. Mwaiselage amesema huduma hiyo lazima itolewe kwa mujibu wa daktari na sio kutumia vinginevyo na nchi nyingi zimeweza kutumia dawa hizo wamekuwa na mfanikio.

Dk. Mwaiselage amesema kuwa wagonjwa wa saratani wanapitia katika hatua nne ambazo ya kwanza mtu anaweza kutibiwa na kupona na hatua ya pili anaweza kupona kwa asilimia 50 hatua ya tatu na ya nne wagonjwa hao wanakuwa na kiwango cha juu hivyo huduma tiba yao kupata shufaa.

Amesema kuwa wadau wameutengeneza muongozo ili kuweza kutumika kutokana na wagojwa asilimia 80 wanahitaji huduma ya tiba ya shufaa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...