Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, akihutubia wanakijiji cha Kipara
Mpakani kabla ya Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Maghembe kukabidhi
eneo la hekali 50 kwa kijiji hicho kwa ajili ya huduma za kijamii.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, akihutubia wanakijiji cha Kipara Mpakani katika mkutano huo kabla ya makabidhiano.
Mzee wa Kijiji cha Kipara Mpakani akimshukuru Waziri wa Maliasili na
Utalii, Profesa Jumanne Maghembe na Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega,
kwaniaba ya wanakijiji hicho.
Na Mwandishi Wetu.
SERIKALI
imerejesha eneo la hekeli 50 Kwa wananchi wa kijiji cha kipara mpakani
kilichopo Kata ya Mwandege,Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani ili wajenge
huduma za kijamii.
Akikabidhi
eneo hilo Waziri wa Maliasi na Utalii Profesa Jumanne Maghembe
aliwaeleza wananchi hao ambo walijitokeza Kwa wingi katika mkutano
amesema kuwa wamponge Mbunge wa Jimbo hilo Abdallah Ulega kwani
amefanya jitihada kubwa za kuhakikisha Serikili inatoa Kwa wananchi eneo
hilo.
Amesema
kuwa wakati wako Bungeni mbunge huyo pamoja na baadhi viongozi wa kata
hiyo walikwenda Bungeni na kuiomba Serikali kuwapa eneo hilo ambapo
lilikuwa pori tengefu la maliasili ili wananchi wa kata ya Mwandege
waweze kujenga Masoko.Shule,na miundombinu mingine.
"Nawapa
eneo hili leo kwaniaba ya Serikali kwani najuwa Mh.rais Dkt.Magufuli
wakati wakampeni alipita hapa nakuzungumzia eneo hili hivyo tunahitaji
mjenge huduma mbalimbali na sio baadae watu wajitokeze na kusema eneo la
kwenu."amesema Profesa Maghembe.
Naye
Mbunge Ulega akizungumza katika mkutano huo amesema kuwa wananchi hao
niwastaratibu kwani.mbali na kukosa maeneo ya kujenga huduma za jamii
bado walikuwa wamekituza eneo hilo hadi leo Serikali wanapoamua kuwapa
wananchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...