dre
Mwanafunzi  aliyeongoza masomo yote Rahma Mdea akipokea cheti cha kuhitimu darasa la  saba na zawadi yake  wakati wa mahafali ya  shule ya  Southern Highlands Mafinga

Mwanafunzi  aliyeongoza masomo yote Rahma Mdeka akipokea cheti cha kuhitimu darasa la  saba na zawadi yake  wakati wa mahafali ya  shule ya  Southern Highlands Mafinga mkur
 Mkurugenzi wa shule za Southern Highlands Mafinga ,Mary  Mungai  kulia akitambulisha watumishi  wa  shule  hiyo.
………………………………….
Na MatukiodaimaBlog 

UONGOZI wa  shule ya  Southern Highlands Mafinga  wilayani  Mufindi umewataka wazazi  wa  wanafunzi zaidi ya 50 waliofanya mtihani wa Taifa  wa darasa la  saba katika shule   hiyo  kuanza  kuwa na uhakika  wa watoto wao  kufaulu mtihani   huo .


Huku ukiahidi  kutoa kuchangia sehemu ya ada kwa  wanafunzi watakajiunga na shule ya sekondari  ya  Southern Highlands Mafinga kama  sehemu ya ahsante kwa  ushirikiano  ambao  wazazi  wamekuwa  wakitoa kwa shule hizo.

Mkurugenzi mtendaji wa Southern Highlands Mafinga  Mary  Mungai  aliyasema haya jana  wakati wa mahafali ya darasa  la  saba  shuleni  hapo .


“Shule hii ilianza mwaka 1994 kama Day Care na Pre-School. Mwaka 1997 ikakuwa na kuanza shule ya msingi-Primary School mwaka 2001 shule ilitoa wanafunzi wa kwanzawa darasa la saba wanafunzi walikuwa 17,wote walifauru vizuri na wote  walichaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza Katika matokeo ya mitihani ya darasa la 7 ya mwaka 2001 Southern Highlands School ilishika nafasi ya kwanza kitaifa katika mitihani yasomo la kiingereza ”


Alisema kuwa matokeo mazuri ya wanafunzi wote kufaulu mitihani ya kitaifa ya darasa la saba yamekuwa ni kawaida  kwa  shule   hiyo na  kuwa  toka kuanzishwa kwake haijapa pata  kufelisha hata  mwanafunzi  mmoja .

Hivyo kuwataka  wazazi  kutokuwa na hofu  juu ya  wanafunzi hao  waliofanya mtihani mwaka  huu kwani waanze  kujiandaa kwa kuwapeleka  sekondari.


Wakati huo   huo mkurugenzi wa familia  ya Lucy Chawe inayoishi nchini marekani na Tanzania  imepongeza jitihada za  shule  hiyo na  kuahidi kuendelea  kuiunga mkono  serikali kwa  kuhamasisha masomo ya Sayansi na Hisabati kwa  wanafunzi 

Mkurugenzi wa The Chawe Foundation Award , Kitove Mungai  alisema  kuwa  kila mwaka  wamekuwa wakitoa  zawadi kwa  wanafunzi wa Awali   hadi  darasala  saba ambao wamekuwa  wakifanya vizuri masomo ya  Hisabati na sayansi .


Aliwataja wanafunzi  ambao  wamepewa  zawadi hiyo kwa mwaka  huu kuwa ni Brayan Mgomapayo, Rahma Mdeka na Ayub Toss ambao  walifanya  vizuri katika hesabu .


Wakati katika  sayansi wanafunzi waliopewa  zawadi ni  Nimrod Nyakunga , Rahma Mdeka na Erick Mwanjelwa .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...