Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Kongwa  Mh. Mhe. Job Ndugai; leo amekuwa miongoni mwa viongozi waliokabidhiwa Kitambulisho cha Taifa chenye muonekano mpya, baada ya kutembelea eneo ambapo waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamekuwa wakisajiliwa na kugawiwa vitambulisho vya Taifa vyenye muonekano mpya.

Akikabidhi Kitambulisho hicho, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Iramba Magharibi Mhe. Mwigulu Nchemba; amesema hatua ilivyofikiwa sasa na Serikali ni kuona zoezi la Vitambulisho vya Taifa linakamilika na kuanza kuwa chachu katika kuleta maendeleo na suluhisho katika huduma nchini zenye kuhitaji utambuzi.

Amesema Kitambulisho cha Taifa kina umuhimu mkubwa katika maendeleo, ustawi na usalama wa Taifa; hivyo hakuna budi kuhakikisha mipango ya utekelezaji inakamilika ili kutoa wigo mpana wa matumizi ya Vitambulisho pamoja na kuunganisha mifumo ya Serikali kubadilishana taarifa kwa lengo la kuleta ufanisi zaidi katika utoaji huduma kwa jamii

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa kitambulisho chake; Mh. Spika amepongeza kazi nzuri inayofanywa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa; na kutoa wito wa kuharakishwa kuunganishwa kwa  mifumo mingine ya Serikali na NIDA  ili kusaidia Serikali kufikia kwa haraka malengo iliyojiwekea kwa wananchi na kuimarisha ulinzi na usalama wa Taifa
Wengine waliopewa vitambulisho leo ni pamoja na Mh. Tulia Akson Mwansasu Naibu Spika, Mawaziri Naibu Mawaziri, wabunge na baadhi ya wafanyakazi wa Bunge 
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Kongwa Mhe. Job Ndugai akipokea Kitambulisho chake chenye saini kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mwigulu Nchemba katika makabidhiano mafupi yaliyofanyika Bungeni Dodoma leo
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Kongwa Mhe. Job Ndugai akiweka saini kitabu cha kumbukumbu baada kupokea Kitambulisho chake Bungeni Dodoma Leo. Kulia ni Afisa Usajili wa Wilaya ya Dodoma Mjini Bwana. Khalid Mrisho.
 Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Hifadhi Hati NIDA Bi. Rose Mdami akitoa maelezo kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Kongwa Mhe. Job Ndugai kuhusu shughuli za ugawaji Vitambulisho vya Taifa zinazoendelea kwa waheshimiwa Wabunge mjini Dodoma.  Katikati ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mwigulu Nchemba
Watumishi wa NIDA wakitoa huduma ya ugawaji vitambulisho vyenye saini kwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bungeni Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...