KILIMANJARO QUEENS NEEMA TUPU
Ubingwa Kombe la CECAFA Chalenji kwa timu za mpira wa miguu za wanawake katika nchi za Afrika Mashariki, umewavutia wadau wengi kwa kiwango kikubwa hivyo kushusha neema kwa wachezaji hao wa timu ya taifa ya Tanzania Bara maarufu kama Kilimanjaro Queens ambayo imeandika historia ya kutwaa taji hilo ikiwa ni taifa la kwanza katika mashindano hayo mapya.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amefurahishwa na ubingwa wa timu hiyo akisema: “Si ubingwa tu, bali umefuta dhana ya Wakenya ambao siku zote wamekuwa wakitangaza Mlima Kilimanjaro uko kwao Kenya wakati upo hapa Tanzania. Kwa kuifunga Kenya, mmefanya kazi nzuri.”

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

LIGI DARAJA LA KWANZA YAANZA
Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inaanza wikiendi hii ambako katika kundi A, mchezo wa kwanza unapigwa leo Ijumaa Septemba 23, 2016 kwa kuzikutanisha timu za Ashanti United ya Ilala, Dar es Salaam na Pamba ya Mwanza katika mchezo utakaopigwa Uwanja wa Karume jijini.
Kwa mujibu wa ratiba, michezo mingine itachezwa kesho Septemba 24, 2016 kwa kuzikutanisha timu za Lipuli dhidi African Sports utakaofanyika Uwanja wa Kichangani mjini Iringa. Mchezo huo utakuwa ni wa kundi A wakati katika kundi B michezo itakuwa ni kati ya Kurugenzi ya Iringa dhidi ya KMC ya Kinondoni kwenye Uwanja wa Wambi ulioko Mafinga. Mlale JKT itaikaribisha Njombe Mji kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

KAMATI YA KATIBA, SHERIA KUJADILI KESI 13 KESHO
Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za wachezaji kesho Jumamosi Septemba 24, 2016 itasikiliza mashauri 13.
 Malalamiko hayo ni:
Mchezaji Ametre Richard ambaye atawasilisha mbele ya kamati makubaliano waliyokubaliana kukaa pamoja na kufikia mafaka. 
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

YANGA, JKT RUVU SASA KUCHEZA OKTOBA 26
Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imepanga mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Young Africans dhidi ya JKT Ruvu, sasa utachezwa Oktoba 26, 2016 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar s Salaam.
Pamoja na mchezo huo, Bodi imefanya mabadiliko katika baadhi ya ya michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom kama ifuatavyo ambako Mwadui na Azam sasa utachezwa na Novemba 9, 2016 siku ambayo Prisons itaikaribisha Simba kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya. Novemba 10, kutakuwa na mchezo kati ya Young Africans dhidi ya Ruvu Shooting jijini Dar es Salaam.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...