Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu |
Na
Eleuteri Mangi, MAELEZO, Bukoba.
Serikali
imesema gharama za kujenga upya shule za sekondari za Ihungo na Nyakato ni Sh.
Bilioni 60 hadi kukamilika miundombinu yake ambayo itakayoruhusu wanafunzi
kupata elimu kama kawaida.
Hayo
yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu leo mjini
Bukoba alipokuwa akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu hatua
zilizochukuliwa na Serikali katika kukabiliana na athari zilizosababishwa na
tetemeko la ardhi lililoukumba mkoa huo.
Katika
kukamilisha ujenzi wa shule hizo, Mkuu wa mkoa amesema kuwa hatua ya kuvunja
majengo yote imeshaanza ambapo tayari Kampuni ya CHICO ya Wachina inaendelea na
uvunjaji wa majengo yote ili kazi ya ujenzi uanze..
“Wataalam
wote wa ujenzi kutoka idara mbalimbali za Serikali wanaendelea na uchambuzi
yakinifu wa majengo mapya ya shule hizo utakaozingatia viwango vya ujenzi
ambapo ghrama za awali kwa tathmini iliyotolewa na wataalamu hao ni Sh. bilioni
30 kwa shule za Ihungo na Nyakato” alisema Meja Jenerali Mstaafu Kijuu.
Uamuzi
wa kuzijenga shule hizo upya zilizoharibiwa na tetemeko la ardhi, ulipelekea
Serikali kuzifunga na kuwahamisha wanafunzi waliokuwa wanasomea katika shule za
Sekondari Ihungo na Nyakato ili waweze kuendelea na masomo wakati shule zao
zinajengwa upya.
Wanafunzi
wa shule hizo tayari wamepangiwa shule watakazoenda ili kuendelea na masomo
kulinhgana na mihula ya mwaka na ratiba za vipindi vya masomo kila siku.
Aidha,
Mkuu huyo wa mkoa amesma kuwa katika kuhakikisha ujenzi wa majengo ya taasisi
za Serikali na wananchi yanakuwa imara na salama, wataalam wa Wakala wa
Jiolojia Tanzania ndio watatoa ushauri wao kabla ya ujenzi mpya haujaanza ili
ujenzi wa majengo mapya ufanyike sehemu sahihi.
Kuhusu
misaada inayotolewa na Serikali, nchi rafiki, wadau na wananchi, Mkuu wa Mkoa
amesema kuwa Kamati ya Maafa katika kukabiliana na athari za tetemeko kwa
wananchi walioathirika tayari imetoa mahitaji mbalimbali kwa waathirika wa
tetemeko hilo.
Mahitaji
yaliyotolewa kwa wananchi ni pamoja na unga wa sembe kilo 3,450, sukari mifuko
410, mchele kilo 3,150, maharage kilo 5,753, maji katoni 850, sabuni katoni 24,
mashuka 90, mablanketi ya watu wazima na watoto 2,020, vyandarua 1,274, sare za
wananfunzi 570, magodoro 694, mahema 127 na matrubali 2,760.
Aidha,
mkuu huyo wa mkoa amezitaka Kamati za Maafa za Wilaya zikarabati miundombinu ya
kutolea huduma za kijamii ikiwemo shule za sekondari na msingi, vituo vya
kutolea huduma za afya vilivyoharibiwa na tetemeko la ardhi ili huduma hizo
muhimu ziweze kurejea mara moja na kutoa huduma kwa wananchi.
Hadi
sasa wamebaki jumla ya majeruhi 13 ambapo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa
wamebakia majeruhi tisa, Hospitali ya Mugana majeruhi wawili na Hospitali ya
Rufaa ya Bugando majeruhi wawili ambao wanaendelea kupata huduma za matibabu na
hali zao zinaendelea vizuri.
Tetemeko
la ardhi lililotokea Septemba 10, 2016 Mkoani Kagera lilisababisha vifo vya
watu 17, majeruhi 440, majeruhi 427 tayari wametibiwa na kuruhusiwa katika
Hospitali ya Rufaa ya mkoa na vituo mbalibali vya afya kwenye mkoa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...