Familia ya Mzee Kangero inasikitika kutangaza kifo cha baba yao Mzee Alfan Kahema Kangero (97) ambaye amefariki nyumbani kwake Kisangara Mwanga. Mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa mwanae mkubwa ADA Estate jijini Dar es salaam na Kisangara.
Maziko yanayarajiwa kufanyika mwisho wa juma kutegemea mafanikio ya safari kwa watoto na ndugu walio nje ya nchi.
Habari ziwafikie ndugu, jamaa, marafiki na majirani popote walipo.
BWANA ALITOA, NA BWANA AMETWAA.
JINA LAKE NA LIHIMIDIWE...
AMEN
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...