Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (wane kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wa Chama cha Waagizaji Wakubwa wa Mafuta (TAOMAC) baada ya kupokea hundi ya fedha kiasi cha sh. Milioni mia nne na nne na laki nane (404,800,000) pamoja na mifuko ya simenti 1000 kutoka chama hicho kwa ikiwa ni mchango wa wanachama wa chama hicho kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa tetemeko la ardhi lililotokea hivi karibuni mkoani Kagera. Wengine ni pamoja na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji ,Charles Mwijage (wa kwanza kulia).

========  ======= ========


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amepokea fedha kiasi cha sh. Milioni mia nne na nne na laki nane (404,800,000) pamoja na mifuko 1000 ya simenti kutoka kwa Chama cha Waagizaji Wakubwa wa Mafuta TAOMAC ikiwa ni mchango wa wanachama wa chama hicho kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa tetemeko la ardhi lililotokea hivi karibuni mkoani Kagera.

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo Waziri Mkuu Majaliwa pamoja na kuwashukuru watu binafsi, taasisi na mashirika yaliyojitoa kwa hali na mali katika kuwasaidia waathirika wa janga hilo, pia aliwahakikishia kuwa misaada wanayoitoa itawafikia walengwa huku akibainisha kuwa serikali imejipanga kuzuia kila aina ya wizi au ubadhilifu wa misaada hiyo.

“Tayari tumechukua hatua kwa wahusika wote waliojaribu kucheza na misaaada hii. Niwahakikishie tu kwamba serikali ipo makini kwenye misaada na michango inayoendelea kutolewa kwa kuwa ni jukumu lake kufanya hivyo kwa kuwa mnapotoa misaada hii maana yake kuna sehemu mmejinyima,’’ alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TAOMAC Bw Salum Bisarara alisema mchango huo ni mwitikio wa ahadi walioyoitoa kwenye mkutano ulioitishwa na Waziri Mkuu Majaliwa na kufanyika Ikulu Septemba 13 nakuhusisha wadau mbalimbali nchini kwa kusudio la kuchangia waathirika wa tetemeko hilo.

“Katika kikao kile Wanachama wa TAOMAC tuliahidi mambo mawili, kwanza wanachama wenzetu watatu ambao ni GBP, OILCOM na MOIL waliahidi kuchangia kwa kuchukua jukumu la kuzijenga upya shule mbili za sekondari zilizoathirika ambazo ni shule ya IHUNGO na ya NYAKATO. Gharama za ujenzi huo tutajulishwa baada ya kukamilika tathmini,’’

“Pili wanachama waliosalia tuliahidi kukutana na kuchangisha fedha ili zisaidie waathirika wa tetemeko kwa njia mbalimbali ikiwemo kutengeneza upya miundo mbinu iliyoharibika hasa zahanati, hospitali, barabara na madaraja, ahadi ambayo tunaikamilisha leo,’’ alisema.

Katika mchango huo jumla ya Sh. Milioni mia mbili na arobaini na nne (244,000,000) tayari zilikuwa zimeingizwa kwenye akaunti maalumu ya kuchangia waathirika hao huku kiasi cha sh milioni mia moja na sitini ((160,000,000) kikiwa ni hundi halisi za kampuni wananchama ambazo zilikabidhiwa kwa mhasibu ofisi ya Waziri Mkuu.

Aliyataja makampuni yalichongia kuwa ni pamoja na Mogas Tanzania Ltd, National Oil (T) LTD, Barrel Petrol Energy, ATN Petroleum Company LTD, Petroafrica (T) Ltd, TSN Oil, Delta Petroleum, Engen Petroleum, Agusta Energy, Petrofuel, Genera Petroleum, Sahara, TIPER, Hass Petroleum, Lake Oil, Dalbit Petroleum, Camel Oil, Gapco, Oryx Oil Company na Puma Energy.

Aidha, wanachama wa chama hicho walimuahidi Waziri Mkuu kuwa wataendelea kuunga mkono juhudi za serikali katika ujenzi wa taifa letu huku wakiishukuru serikali kwa kuwashirikisha katika kuwasaidia waathirika wa tetemeko hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...