Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) umetangaza kusogeza mbele kwa siku moja safari ya treni ya abiria ya Jumanne kwenda bara kutoka Dar es  Salaam. Treni hiyo itaondoka Jumatano  Septemba 14, 2016 saa 9 alasiri.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo sababu za kusogezwa mbele ni kutokana na kipande cha treni kuitoka Kigoma kuchelewa kufika Tabora. Treni hiyo wakati ikienda Kigoma ilicheleweshwa kufika Kigoma baada ya treni ya mizigo kupata ajali kati ya stesheni za Kazuramimba na Luiche..

Uongozi wa TRL unawaomba radhi abiria na wananchi kwa ujumla kwa usumbufu utakaojitokeza
Atakayesoma taarifa hii amwarifu mwenzake.


Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa niaba ya 
Mkurugenzi Mtendaji wa TRL,
 Ndugu Masanja Kungu Kadogosa
Dar es Salaam,
Septemba 12, 2016

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...