Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Msaafu Damian Lubuva akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada walipotoka kwenye mkutano wa 18 wa Tume za Uchaguzi katika nchi zilizo Kusini Mwa Jangwa la Sahara (SADC), uliofanyika Mjini Gaborone-Botswana. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha habari na Mawasiliano wa Tume ya Uchaguzi Tanzania, Clerence Nanyaro.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
TUME ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) ni moja ya Tume kati ya tume za Afrika ambayo imekuwa mfano wa kuifwa katika uchaguzi kutokana kila unapofanyika uchaguzi umekuwa wa huru na haki.

Akizungumza na waandishi habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema kuonekana kwa tume hiyo ni katika mkutano wa 18 wa Tume za Uchaguzi katika nchi zilizo Kusini Mwa Jangwa la Sahara (SADC), uliofanyika Mjini Gaborone-Botswana,  amesema katika mkutano huo Tanzania imekuwa mfano wa kuigwa katika usimamizi wa uchaguzi na kufanya nchi zingine zifanye mfumo huo.

Lubuva amesema kuwa Tume za Uchaguzi katika nchi za SADC zimekuwa zikifanya kwa kutumia vitambulisho vya taifa tofauti na Tanzania kutumia kitambulisho cha mpiga kura lakini uandikishaji wa muda mfupi.

Amesema kuwa Tanzania ziliwakilishwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) pamoja na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) ambapo kwa pamoja zimeonekana kuendesha uchaguzi wa haki na amani.

Aidha amesema kuwa katika mkutano huo nchi za Afrika  zimeonekana kila uchaguzi ukiisha walioshindwa huwa hawakubali matokeo katika chaguzi mbalimbali.

Lubuva amesema kuwa vitambulisho vya taifa vikikamilika kwa kila mtanzania kuwa na kitambulisho kuangalia namna ya kutumia katika chaguzi zijazo.

Hata hivyo amesema mkutano huo Tanzania kupitia NEC zimeweza kujifunza baadhi ya vitu katika uendeshaji wa uchaguzi na wataendelea kufanyia kazi katika kuboresha chaguzi zijazo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Kwa NEC pamoja na mapungufu yake ya upendeleo kwa CCM naweza kukubali walifanya vizuri lakini siyo ZEC ya Jecha......Hapo lazima mseme ukweli ndugu zangu.Anayeisifu ZEC basi ana tatizo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...