Serikali ya Uingereza inatarajia kutoa takribani TZS 6.3 bilioni (sawa na Paundi 2.23 milioni) kusaidia ukarabati wa shule baada ya athari za tetemeko la ardhi mkoani Kagera mnamo Septemba 10.
Msaada huu wa ziada umetangazwa mapema leo wakati Balozi mpya wa Uingereza nchini Tanzania, Sarah Cooke alipokuwa akikabidhi hati ya kibalozi kwa Mheshimiwa Rais wa Magufuli.
Hii ikifuatiwa na ziara iliyofanywa na Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako akiambatana na Mkuu wa Idara ya Kimataifa ya Maendeleo ya Uingereza (DFID), Ndugu Vel Gnanendran.
Misaada hii itatumika katika kukarabati, kuboresha na kuwezesha Shule ya Sekondari ya Ihungo kuwawezesha zaidi ya wanafunzi 740 kuendelea na masomo yao mapema iwezekanavyo. Kwa kuongezea, Serikali ya Uingereza itasaidia pia kukarabati nyumba za walimu katika shule ya Sekondari ya Wasichana ya Rugambwa ambazo zilianguka. Shule hizi ndizo ambazo zimeathiriwa zaidi katika tetemeko la ardhi.
Balozi Mpya, Sarah Cooke alisema; “Serikali ya Uingereza inapenda kutoa salamu zake za masikitiko kwa wale wote ambao wameathirika na tetemeko la ardhi Kagera. Tunaona ni muhimu sana kusaidia Wizara ya Elimu mapema iwezekanavyo ili kuwawezesha watoto wa Bukoba wasiendelee kuangaika zaidi na kuweza kuendelea na masomo yao ndani ya muda mfupi iwezekanavyo.
Hivyo basi, tunapenda kutangaza rasmi kwamba Uingereza itatoa msaada wa ziada kusaidia elimu iendelee kutolewa hasa katika kipindi hiki cha athari za tetemeko Bukoba” Serikali ya Uingereza itadumu imara katika kutoa ushirikiano kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika jitihada zake za kuboresha elimu kwa watoto wote wa Tanzania.

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupoka msaada wa Shilingi Bilioni 6.3 kutoka Idara ya Maendeleo ya Nje ya nchini Uingereza (DFID) ikiwa ni sehemu ya kusaidia Shule zilizoathirika na tetemeko la Ardhi mkoani Kagera leo jijini Dar es Salaam. kushoto ni Mkuu wa Idara ya DFID hapa nchini, Vel Gnanendran.
Mkuu wa Idara ya DFID hapa nchini, Vel Gnanendran akizungumza na waandishi wa habari juu ya Serikali ya Uingereza kutoa msaada wa Shilingi Bilioni 6.3 wenye lengo la kusaidia wahanga wa tetemeko la ardhi hususan kwa shule zilizoathiriwa na tetemeko hilo. kulia ni Waziri wa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Profesa Joyce Ndalichako. Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...