Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameendelea kuwa miongoni mwa wananchi walioanza kuchukua Vitambulisho vipya vya Taifa vyenye saini; kufuatia utaratibu uliotangazwa hivi karibuni na Nida wa kuanza kugawa vitambulisho vipya kwa makundi mbalimbali waliokamilisha taratibu za usajili.  
            Shughuli ya kugawa Vitambulisho vya Taifa kwa Waheshimiwa Wabunge zimeendelea katika siku ya pili bungeni Dodoma; pamoja na kuwasajili wabunge ambao kwa sababu moja au nyingine hawakusajiliwa wakati wa zoezi la awali la usajili.
          Mbali na waheshimiwa Wabunge; wengine ni wafanyakazi wa Bunge na watumishi katika taasisi na Wizara mbalimbali ambao walisajiliwa katika utaratibu wa kawaida wa Usajili. Zaidi ya waheshimiwa Wabunge 240 watapatiwa vitambulisho vyao.
            Zoezi la ugawaji wa Vitambulisho vya Taifa linaendelea katika ofisi zote za usajili za Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa kwa wale wananchi ambao hawakuwahi kupata vitambulisho awali. Kwasasa hakutakuwa na kubadilisha vitambulisho vya zamani kwa wale waliokwisha pata awali kwani Vitambulisho vya zamani vitaendelea kutumika sambamba na vipya katika matumizi mbalimbali  yaliyokusudiwa
 Waziri wa Nishati na Madini na Mbunge wa jimbo la Musoma, Mhe.Profesa Sospeter Muhongo akipokea Kitembulisho chake cha Taifa chenye saini kwa furaha kubwa kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Na Hifadhi Hati NIDA. Bi. Rose Mdami
 Mheshimiwa Waziri wa Katiba na na Sheria Dk. Harrison Mwakyembe, akiwa mwenye furaha kubwa baada ya kuchukua Kitambulisho chake kipya Bungeni Dodoma. NIDA imeanza kutoa vitambulisho vipya vyenye saini kwa viongozi wakiwemo Waheshimiwa Wabunge zoezi linaloedelea mkoani Dodoma sambamba na kikao cha Bunge. 

 Mheshimiwa Deo Sanga, akieleza faida ambazo tayari ameshazipata kwa kutumia Kitambulisho chake cha Taifa. Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Hifadhi hati NIDA Bi, Rose Mdami. Mhe. Sanga amepokea kitambulisho chake leo katika Ofisi za Bunge Dodoma
 Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakipata huduma kutoka kwa maafisa wa NIDA ambao wapo bungeni hapo kutoa vitambulisho vipya kwa waheshimiwa wabunge Mjini Dodoma.
Mbunge wa Muheza na Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama ya Bunge Mheshimiwa Adadi Rajabu akipokea kitambulisho chake kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Hifadhi Hati NIDA Bi. Rose Mdami katika Ofisi za Bunge Mjini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...