Moto mkubwa ulizuka katika uwanja wa ndege wa Nduli manispaa ya Iringa leo. Moto huo inasemekana ulisababishwa na uchomaji mashamba yaliyopo jirani na uwanja huo. Kikosi cha zimamoto kilifanikiwa kuzima moto huo ambao ungeweza kuteketeza vifaa muhimu ikiwa ni pamoja na majengo. 
Akizungumza katika eneo la tukio Mkuu wa wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela (pichani na fulana nyekundu) ambaye alishirikiana na kikosi cha zimamoto kuzima moto huo alisema lazima wananchi wajue kutenga mashamba yao na  kuzuia mioto kusambaa
"Kuanzia sasa yoyote atakaye sababisha moto kutoka kwenye shamba lake atachukuliwa hatua kali za kisheria", alisema Mhe. Kasesela. 
Mkuu wa wilaya huyo piaaliagiza manispaa itengeneze kwa kutumia bullodozer barabara ya kuzuia moto kuzunguka uwanja. Moto huo ulianza majira ya saa 7 mchana na kusambaa hadi kwenye uwanja wa kuondokea ndege (Runway) na  kusogelea eneo la kuhifadhia mafuta ya ndege na vifaa vya kuongozea ndege. Ulidhibitiwa na Jeshi la Zimamoto vizuri na hadi kufikia saa 9.43 moto ulikuwa umezimwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Dah Kasesela.......we acha tu

    ReplyDelete
  2. Mtu wa kujituma huyu. Born leader. Huyu ni kiongozi sio Boss.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...