Youth Climate Activist Network (YouthCAN) Tanzania Ni mtandao wa vijana wanaotoka kwenye taasisi za dini mbalimbali wanaofanya shuguli mbalimbali za mazingira na afya kwa ujumla kwa kujitolea chini ya Shirika la Norwegian Church Aid (NCA)

Kuanzia Tarehe 11/9 /2016 vijana hawa walianza masafara wa Kutembelea baadhi ya maeneo yaliyo athirika sana na mabadiliko ya tabia nchi. Ili kutoa elimu ya Utunzaji wa mazingira, vyanzo vya maji na usafi .baada ya kutoa elimu hiyo Halmashauri ya wiliya Kishapu Mkoani Shinyanga wanatarajia kwenda Kutoa elimu hiyo Mkoani Manyara kwenye baadhi ya vijiji vilivyopo Hanang.Hydom na Mbulu.

Licha ya kutoa elimu juu mazingira,Maji ana afya vijana hawa watapata nafasi ya kuzindua baadhi ya Visima vya maji vilivyo jengwa na Shirika la Norwegian Church Aid (NCA) kwa kushirikiana na Washirika wake.

Ambapo kwa kuanza wamepata fursa ya kushiriki uzinduzi wa visima 7 vilivyojengwa kwa msaada wa watu wa Norway visima hivyo vitasaidia kutatua tatizo la maji safi na salama katika vijiji vi 3 wiliyani Kishapu .ambavyo ni IKONDA A,UBATA na MWAWEJI.

Mkurugenzi wa Halimashauri ya Wilaya Kishapu Bwana.Stephen M Magoiga akizindua moja kati ya Visima saba.

Afisa Mradi Mwandamizi Mama Tina Mosha Akimtwisha maji Moja ya wanakiji wa IKONDA.
Nizar Selemani Mratibu wa shuguli za vijana katika shirika la NCA na Baraka Chedego ambae ni Mratibu wa Youth CAN wakizungumza jambo wakati wa mkutano na wanakijiji cha Ikonda.
Moja visima vilivyokuwa vikitumiwa na wanachi kabla ya ujenzi wa visima vya kisasa.
Picha zote na IMANI SELEMANI NSAMILA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...