Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano, Luhaga Mpina
akipanda mti katika Shule ya Sekondani ya Mama Salma Kikwete, Jijini Dar es
Salaam leo ikiwa ni kuunga mkono kampeni ya upanadaji miti Jijini Dar es Salaam iliyoanzishwa na Mkuu wa Mkoa huo Paul
Makonda, Kampeni hiyo ijulikanayo kama "Mti Wangu" itazinduliwa kesho
Oktoba Mosi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.
Samia Suluhu Hassan. Wakala wa Huduma za Misitu
Tanzania umechangia miche ya miti 600 katika shule hiyo na miche ya miti
mingine 3,000 itatolewa kesho wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo kwa
ajili ya Jijiji la Dar es Slaam, katika awamu ya pili watachangia tena
miche ya miti 5,000.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano, Luhaga Mpina
(wa pili kulia) akimkabidhi Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mama Salma Kikwete,
Elestina Chanafi (wa pili kushoto) baadhi ya miche ya miti kati ya miche 600 iliyotolewa na Wakala wa
Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa ajili ya shule hiyo kuunga mkono Kampeni ya
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ya upandaji wa miti Jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Prof. Dos Santos Silayo.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos
Santos Silayo (kulia) akimkabidhi Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais
Mazingira na Muungano, Luhaga Mpina (wa pili kulia) miche 600 ya miti iliyotolewa na ofisi yake kwa ajili
ya shule ya Sekondani ya Mama Salma Kikwete Jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni hatua
ya kuunga mkono Kampeni ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ya upandaji wa miti Jijini Dar es Salaam ijulikanyo
kama “Mti Wangu” . Katika uzinduzi huo
TFS imechangia miche ya miti 3,000 kati ya miche 8,000 ambayo imepanga kutoa
kwa ajili ya kupandwa katika Jiji la Dar es Salaam.
Kaimu
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos
Santos Silayo akizungumza na waandishi wa habari katika hafla hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...