Meneja
wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshack Bandawe akizungumza
na wanachama wa mfuko huo jijini Mwanza jana kabla ya kuwakabidhi kadi
za matibabu ya mfumo wa uchangiaji wa hiari(Wote Scheme).
Na Baltazar Mashaka,Mwanza
WANACHAMA
106 kati ya 7, 185 wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa kupitia
mfumo maalum wa uchangiaji wa hiari wa WOTE Scheme wamekabidhiwa kadi
zitakazo wawezesha kupata huduma za matibabu.
Akikabidhi
kadi hizo kwa wanachama hao, Meneja wa PPF Kanda ya Ziwa Meshach
Bandawe alisema mfumo huo umewalenga wanachama waliojiajiri wenyewe
katika Sekta isiyo rasmi ambao kwa mujibu wa takwimu za kitaifa ni zaidi
ya asilimia 90 ya nguvu kazi ya taifa.
Alisema
kuwa bahati mbaya kundi hilo lilisahaulika na halijakingwa kikamilifu
na sekta ya Hifadhi ya Jamii nchini ingawa ni ukweli usiopingika kuwa
wanapatwa na majanga hatarishi sawa na wafanyakazi wa sekta rasmi.
“ Watu waliojiajiri kwenye Sekta isiyo rasmi wanafanya shughuli
mbalimbali za kiuchumi na uzalishaji mali na kuwaingizia kipato cha
uhakika na kumudu kuendesha maisha yao.Bahati mbaya hawana akiba yoyote
wanayoweza kunufaika nayo kwa maisha ya baadaye iwapo wangejiunga na
mifuko ya Hifadhi ya Jamii,” alisema.
Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshack Bandawe
akimkabidhi Anastanzia Magere kadi ya matibabu ya mfumo wa uchangiaji wa
hiari(Wote Scheme) jijini Mwanza jana. Mpaka sasa Kanda hiyo
wamekwishajiunga wanachama 7185 kwa kipindi cha Agosti 2015 mpaka Agosti
2016. Picha na Lordrick Ngowi
Meneja
huyo wa PPF alieleza kuwa mfuko kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa
Bima ya Afya ( NHIF) utatoa huduma ya matibabu kwa wanachama baada ya
kuchangia sh.60,000 na watatibiwa magonjwa yaliyoanishwa kwenye sera ya
kitaifa.
Bandawe
alisema wanachama hao watapata huduma hiyo ya matibabu katika hospitali
zaidi ya 6,000 nchini ambazo zimeingia mkataba na NHIF na wanastahili
kuwa na kadi watakazotumia kupata huduma hizo kwa kipindi cha mwaka
mmoja na akatoa wito kwa makundi mbalimbali yaliyoko katika sekta isiyo
rasmi yajiunge na mfumo huu kwa faida ya maisha yao na wanufaike na
huduma mbalimbali zinazotolewa na PPF .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...