Na.
Immaculate Makilika- MAELEZO
Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki kwa kushirikiana na Ofisi ya
Waziri Mkuu imeandaa matembezi ya hisani ili kusaidia wahanga waliokumbwa na
maafa ya tetemeko la ardhi
lilitotokea Septemba 10 mwaka huu,
huko mkoani Kagera.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es
salaam Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Afrika Mashariki Bi. Mindi Kasiga amesema kuwa, matembezi hayo ya hisani ya
kilomita tano yataongozwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan
Mwinyi.
Aliongeza kuwa Matembezi hayo yatafanyika siku
ya Jumamosi Septemba17 mwaka huu, ambapo yataanzia Bwalo la Polisi Osterbay (Polisi
Officer’s Mess) kuanzia saa 12 asubuhi.
Aidha
amesema kuwa, matembezi hayo yana lengo la kuhamasisha wafanyabiashara, taasisi
za fedha, kampuni mbalimbali pamoja na jamii ya watanzania, wanadiplomasia waliopo
nchini kuchangia kwa kutoa misaada mbalimbali ili kusaidia wahanga maafa ya tetemeko
la ardhi la mkoani Kagera.
“Tunafanya
kampeni hii ya tembea kwa ajili ya Kagera, kwa lengo la kuwahamasisha
watanzania, wafanyabashara na jumuiya ya wanadiplomasia waliopo nchini ili kila
mtu aweze kushiriki kwa kuchangia kiasi chochote cha fedha kitakachosaidia wenzetu
waliokumbwa na maafa ya tetemeko la ardhi lililotokea Kagera” alisema Kasiga
Hivyo
basi, Wizara hiyo imeeandaa daftari maalumu la michango kwa jumuiya ya
mabalozi katika nchi zote zenye Ofisi za
Ubalozi wa Tanzania, ili kuunga mkono zoezi la kuwasaidia wahanga wa maafa ya
tetemeko la ardhi lilitokea mjini Bukoba.
Pia
Serikali imefungua akaunti rasmi kwa jina la Kamati Maafa Kagera katika benki
ya CRDB ya mkoani Kagera yenye namba
0152225617300 ambayo itakayotumika kupokea michango kutoka kwa watu mbalimbali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...