Washiriki wa Miss Temeke 2016 wakifanya mazoezi ya kujiandaa na shindano lao jijini Dar es Salaam. Shindano hilo, litakalofanyika Viwanja vya Sigara TCC Chang'ombe Septemba 24 mwaka huu.


Na Dotto Mwaibale

WAREMBO 16 wanatarajia kupanda jukwaani katika shindano la kumpata Miss Temeke 2016 litakalofanyika Septemba 24 mwaka huu.

Akizungumza Dar es Salaam katika mazoezi yao, Mwalimu wa warembo hao Neema Honest alisema warembo wote wapo fiti na wanaendelea vizuri na mazoezi Chang'ombe Sigara TCC.

"Washiriki wote wapo katika hali nzuri na sasa wanaendelea na mazoezi tayari kwa shindano hilo litakalofanyika Chang'ombe Sigara TCC" alisema Honest.Aliwataja warembo kuwa ni Jesca Nassary, Diana Nyaki, Juliet Pallangyo, Irene Tomitho, Macrina Kudema, Anitha Mugisha, Khadija Masoud na Sia Kiweru.

Aliwataja wengine kuwa ni Sara Bigambo, Nancy Mushi, Mwantum, Esther Mnaki, Anitha Kisimba na Clara Premsinga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...